Kesi ya Uhaini Dhidi ya Tundu Lissu Yaahirshwa Kwa Sababu za Kiusalama
Wakili wa Serikali, Thawabu Issa, akiwasilisha maelezo kwa niaba ya wenzake, alieleza kuwa baada ya kufika mahakamani na kutomuona mshtakiwa, walifanya mawasiliano na Jeshi la Magereza ambapo Mkuu wa Magereza aliwataarifu kwamba Lissu hakuweza kufikishwa mahakamani kwa sababu za kiusalama.