Lissu Ashinda Pingamizi Lingine Kesi Ya Uhaini
Katika pingamizi hilo, Lissu alipinga uwasilishaji wa taarifa hiyo akieleza kuwa shahidi, Mkaguzi wa Jeshi la Polisi Samwel Elibariki Kaaya hana mamlaka ya kisheria ya kuandaa “report” bali “certificate” pekee ya uchunguzi, kwa mujibu wa tangazo la serikali linalomtambua chini ya kifungu cha 216(1) cha Sheria ya Ushahidi.