Waandamanaji wa Madagascar waendelea licha ya kufutwa kwa serikali
Waandamanaji nchini Madagascar wameitisha maandamano mapya leo Jumanne, siku moja baada ya Rais wa nchi hiyo Andry Rajoelina kuvunja serikali yake kwa lengo la kutuliza ghasia zilizosababisha vifo vya watu 22, kwa mujibu wa Umoja wa Mataifa.