Kiongozi wa upinzani Uganda ajificha, mwingine akiwa mahututi hospitalini
Kiongozi wa upinzani nchini Uganda, Bobi Wine, amesema yuko mafichoni kufuatia uchaguzi wa wiki iliyopita, huku kiongozi mwingine wa upinzani, Kizza Besigye, akiwa mahututi kutokana na hali mbaya ya afya, kwa mujibu wa mke wake.