Wakenya wakamatwa wakipinga kituo cha karantini ya Ebola kwa Raia wa Marekani
Kituo hicho kinajengwa katika Kambi ya Anga ya Laikipia, iliyopo Nanyuki chini ya Mlima Kenya, na kinatarajiwa kutumika kuwaweka karantini raia wa Marekani watakaowasili kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC), ambayo kwa sasa inakabiliwa na mlipuko mkubwa wa ugonjwa wa Ebola