Ni nini hatma ya kesi ya Lissu?
Tundu Lissu ni mwanasiasa mkongwe wa upinzani na mmoja wa wakosoaji wakuu wa sera na utendaji wa serikali nchini Tanzania, anakabiliwa na mashtaka ya Uhaini ambayo anadaiwa kuyatenda mnamo mwezi Aprili 2025. Kesi yake imeibua mjadala mpana kuhusu uhuru wa kisiasa, nafasi ya upinzani na mwenendo wa haki katika masuala yanayogusa wanasiasa.