Kesi ya Lissu:Hatima ya vielelezo vya video kesi ya Lissu kujulikana Jumatano
Lissu, ambaye anajitetea mwenyewe, anakabiliwa na shtaka la uhaini yanayodaiwa kutokana na matamshi aliyotoa Aprili 3,2025. Alikamatwa Aprili 9, 2025 mkoani Ruvuma na kisha kusafirishwa hadi Dar es Salaam, ambako anakabiliwa na kesi hiyo mbele ya jopo la majaji wa Mahakama Kuu.