Lissu ajiwakilisha mwenyewe Mahakamani baada ya kunyimwa haki ya kuonana na Mawakili wake Gerezani
Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Tundu Lissu, ameieleza Mahakama ya Kisutu kuwa ameamua kujiwakilisha mwenyewe katika shauri la uhaini yanayomkabili, akidai kunyimwa haki ya kuonana kwa faragha na mawakili wake tangu alipowekwa mahabusu zaidi ya miezi miwili iliyopita.