Mwenyekiti wa walimu wasio na ajira akamatwa
Mwenyekiti wa Umoja wa Walimu Wasio na Ajira Tanzania (NETO), Joseph Paulo Kaheza amekamatwa akiwa mkoani Geita kwa kile kinachodaiwa kuwa ni vuguvugu la kupigania ajira kwa walimu wa Tanzania.
Mwenyekiti wa Umoja wa Walimu Wasio na Ajira Tanzania (NETO), Joseph Paulo Kaheza amekamatwa akiwa mkoani Geita kwa kile kinachodaiwa kuwa ni vuguvugu la kupigania ajira kwa walimu wa Tanzania.
Msemaji Mkuu wa serikali, Gerson Msigwa, amesema kuwa kuanzia mwaka huu, wanahabari nchini Tanzania watatolewa kadi za habari za kidijitali kama sehemu ya mpango wa serikali wa kuboresha sekta ya habari.
Rais wa Chama cha Mawakili Tanganyika (TLS), Boniface Mwabukusi leo Jumanne Februari 18, 2025, kwenye Uzinduzi wa kampeni ya Kitaifa ya msaada wa kisheria ya Mama Samia Jijini Mwanza, ameshauri kuzingatiwa kwa Ibara ya Tisa ya Katiba ya Tanzania yenye kuhimiza kuhusu utu, Upendo na utii kama suluhu ya migogoro mingi ya kijamii.
Ziara ya Rais Samia nchini Ethiopia imeanza leo ambapo anatarajia kuhitimisha Februari 16,2025.
Mapigano yalizuka tena leo Jumanne mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo baada ya mapumziko ya siku mbili, ambapo wapiganaji wa M23 wanaoungwa mkono na Rwanda walishambulia maeneo ya jeshi la Congo katika jimbo la South Kivu asubuhi, kwa mujibu wa vyanzo vya eneo na usalama vilivyosema.
Hii leo inatajwa kwa ajili ya kuangaliwa iwapo upelelezi wa kesi umekamilika, ingawa imefungwa mikono kuendelea na hatua zaidi baada ya Mkurugenzi wa Mashtaka nchini kuwasilisha kusudio la kukata rufaa katika Mahakama ya Rufani kupinga uamuzi wa Mahakama Kuu kuhusu kupatikana kwa dhamana ya mshtakiwa kutokana na kuangalia uhalali wa kesi ya jinai kwa haraka.
Kwa mujibu wa taarifa hiyo iliyotolewa leo, bei ya petroli kwa rejareja katika Jiji la Dar es Salaam imeongezeka kwa asilimia 0.957, dizeli kwa asilimia 2.18 na mafuta ya taa kwa asilimia 1.25.
Wanajeshi wawili wa Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) wameuawa katika mapigano yaliyotokea katika kipindi cha siku kumi zilizopita mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo
Mkutano huo ulifanyika baada ya wanajeshi 16 kutoka Afrika Kusini na Malawi, pia wanachama wa SADC, kuuawa katika mapigano ya karibuni karibu na Goma, ambako walikuwa wamepelekwa kama sehemu ya juhudi za kudumisha amani.
Wasira ametoa mfano wa Donald Trump, ambaye amechaguliwa kuwa Rais wa Marekani katika uchaguzi wa hivi karibuni, akisema kuwa licha ya umri wake mkubwa, Wamarekani walimchagua kwa sababu ya sera zake na si kwa kuangalia umri wake.