Kampeni za urais Tanzania kuanza rasmi huku mgombea wa ACT Wazalendo akizuiwa kugombea
Kwa mujibu wa INEC, jumla ya vyama 18 vilivyosajiliwa vitashiriki uchaguzi huu, na wagombea 17 wa urais watashiriki kinyang’anyiro
Kwa mujibu wa INEC, jumla ya vyama 18 vilivyosajiliwa vitashiriki uchaguzi huu, na wagombea 17 wa urais watashiriki kinyang’anyiro
Ahadi hiyo imetolewa jana katika mazungumzo yake na Rais wa Chama cha Wanasheria Tanganyika (TLS), Boniface Mwabukusi, yaliyofanyika Ikulu ya Chamwino jijini Dodoma.
Katika taarifa yake kwa umma, chama hicho kimeeleza kuwa hatua ya Msajili haina mashiko ya kisheria kwa kuwa mchakato wa uchaguzi tayari umeshaanza, huku Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC) ikiwagawia wagombea fomu za kugombea urais. Kwa mujibu wa ACT Wazalendo, Msajili hana mamlaka ya kuingilia hatua hiyo, zaidi ya kushughulikia malalamiko kwa njia ya pingamizi.
Tume ya Afrika ya Haki za Binadamu na Watu (ACHPR) imeitolea wito Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuhakikisha inalinda, inaheshimu na inatekeleza kwa dhati viwango vya haki za binadamu kuelekea uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika mwezi Oktoba 2025.
Kipindi cha uongozi wake kama Spika kiligubikwa na malalamiko kutoka kwa baadhi ya wanasiasa wa upinzani waliomtuhumu kwa upendeleo, kufungia wabunge waliokuwa wakikosoa serikali, pamoja na kuziba mijadala mizito ndani ya Bunge.
Ingawa majina ya mwisho ya wagombea yataamuliwa na ngazi za juu za chama hicho, matokeo ya sasa yameweka uelekeo wa wazi kuwa sehemu kubwa ya wanachama wameonyesha hamu ya kuona sura mpya zikipewa nafasi ya uongozi.
Gambia imeripoti mlipuko wa ugonjwa wa mpox siku ya Jumanne baada ya kugunduliwa kwa kisa kimoja kupitia mfumo wa kawaida wa ufuatiliaji wa magonjwa, huku nchi kadhaa jirani zikiripoti ongezeko la maambukizi hivi karibuni.
Wakati wengi walitarajia angerejea katika ulingo wa kisiasa kwa mtindo mpya, Mbowe amebaki kivuli cha kile kilichowahi kuwa sauti kali ya upinzani Tanzania.
Agizo hilo, lililotolewa rasmi leo Juni 25, 2025, linanukuu madai ya ukiukaji wa Kifungu cha 33(2) na 34(1) cha Katiba ya Kenya, pamoja na Kifungu cha 461 cha Sheria ya Mawasiliano na Habari ya Kenya (Kenya Information and Communications Act).
Katika taarifa iliyotolewa leo Jumatano tarehe 18 Juni 2025, ambayo imeeleza baadhi ya matukio hayo, polisi wamesema uchunguzi wa kina umebaini kuwa watu wengi waliodaiwa kutekwa ama walikuwa wamejificha kwa hiari, walitoroka kutokana na sababu mbalimbali au walihusika katika vitendo vya uhalifu kabla ya kupotea kwao.