Shahidi wa pili aeleza alivyotambua Jinai kwenye video ya Tundu Lissu
Shahidi wa kwanza alihitimisha ushahidi wake leo baada ya kuhojiwa kwa maswali ya nyongeza na jopo la mawakili wa Serikali
Shahidi wa kwanza alihitimisha ushahidi wake leo baada ya kuhojiwa kwa maswali ya nyongeza na jopo la mawakili wa Serikali
Katika mahojiano hayo, Lissu alitumia takribani saa saba kumuhoji Shahidi huyo kuanzia majira ya saa 3:30 mpaka saa 10, muda wote aliutumia kupima uhalali wa ushahidi wa shahidi huyo, akihusisha masuala mbalimbali kulinga na ushahidi aliouandika katika maelezo yake ikiwamo ya taratibu za kiuchunguzi, matumizi ya notebook ya polisi, video za ushahidi na tafsiri ya maneno yaliyotumika kwenye mashtaka ya uhaini.
Shahidi huyo ambaye ni Kamishina Msaidizi wa Polisi (ACP) George Wilbart Bagemu, mwenye umri wa miaka 48, ambaye ni afisa mwandamizi wa Jeshi la Polisi mwenye uzoefu wa zaidi ya miaka ishirini katika taaluma ya upelelezi.
Goodall, aliyebobea katika utafiti wa sokwe pori na baadaye kuwa mwanaharakati wa mazingira, alibadilisha mapenzi yake ya wanyamapori kuwa kampeni ya maisha yote. Safari yake ilimtoa kutoka kijiji cha pwani kusini mwa Uingereza hadi Afrika, na hatimaye kumzungusha duniani kote akijitahidi kuelewa sokwe na nafasi ya binadamu katika kulinda makazi yao pamoja na afya ya sayari kwa ujumla.
Wanaharakati wa mitandaoni, Innocent Paul Chuwa maarufu kama Kiduku, na Farida Mikoroti, waliokamatwa kwa tuhuma za makosa ya mtandao, wameachiwa kwa dhamana kutoka Kituo Kikuu cha Polisi cha Kati (Central Police) Dar es Salaam, Jumatano Oktoba 01, 2025.
Waandamanaji nchini Madagascar wameitisha maandamano mapya leo Jumanne, siku moja baada ya Rais wa nchi hiyo Andry Rajoelina kuvunja serikali yake kwa lengo la kutuliza ghasia zilizosababisha vifo vya watu 22, kwa mujibu wa Umoja wa Mataifa.
Wiki iliyopita maandamano ya siku mbili yaliibuka na kusababisha makabiliano kati ya vijana na polisi. Waandamanaji, waliyoitishwa kupitia mitandao ya kijamii na vuguvugu la “Gen Z”, walilalamikia kukatika kwa maji na umeme kunakolikithiri katika taifa hilo maskini.
Leo kesi hiyo ilikuja kwa ajili ya kutolewa uamuzi mdogo kuhusu mapingamizi aliyowasilisha Lissu, ambapo alipinga uhalali wa hati ya mashtaka na pia akakosoa maelezo ya mashahidi akidai yameandikwa kinyume cha sheria.
Katika kauli yake ya majibu kwa wito huo, Polepole amesema anauchukulia kwa sura mbili; upande wa kwanza akiwaona Polisi wana dhamira njema ya kusikiliza na kukusanya ushahidi, lakini upande wa pili akihisi kuna mbinu na nia ovu zinazoweza kuhatarisha usalama wake.
Lissu alieleza kutoridhishwa kwake na namna Wakili wa Serikali alivyomtaja kama “mwenzetu”, akisisitiza kuwa hana uhusiano wowote na upande huo wa mashtaka.