Maandamano ya kupinga serikali Madagascar yazuka upya, polisi watumia gesi ya machozi
Wiki iliyopita maandamano ya siku mbili yaliibuka na kusababisha makabiliano kati ya vijana na polisi. Waandamanaji, waliyoitishwa kupitia mitandao ya kijamii na vuguvugu la “Gen Z”, walilalamikia kukatika kwa maji na umeme kunakolikithiri katika taifa hilo maskini.