Jumba la maonyesho Ukraine, lililowapa hifadhi zaidi ya raia 1,000 lalipuliwa kwa mabomu
Zaidi ya watu 2,000 wameuawa katika mji huo wa Mariupol kulingana na mamlaka ya Ukraine.
Zaidi ya watu 2,000 wameuawa katika mji huo wa Mariupol kulingana na mamlaka ya Ukraine.
Bei ya unga wa mahindi, mchele, sukari, mafuta na nyanya imepanda, na hivyo kutoa changamoto kubwa kwa wale wanoishi kwa dola kadhaa kwa siku.
Mwezi huu Urusi ilipitisha vifungo vya sheria vya kifungo cha hadi miaka 15 jela kwa kueneza habari za uwongo zenye lengo la kudhalilisha jeshi lake, pamoja na kifungo cha hadi miaka 3 jela kwa kuitisha vikwazo dhidi ya Urusi.
Kremlin ilisema wiki iliyopita kwamba watu wa kujitolea, wakiwemo kutoka Syria, wanakaribishwa kupigana pamoja na jeshi la Urusi nchini Ukraine.
Msururu wa milipuko mikali ilitikisa maeneo ya makazi ya watu wa Kyiv mapema Jumanne na kuua watu wawili, saa chache kabla ya mazungumzo kati ya Ukraine na Urusi kutarajiwa kuanza tena.
Watumiaji wa mtandao wa Instagram nchini Urusi wamepewa taarifa kuwa huduma hiyo imesitishwa kuanzia saa sita usiku Jumapili ya March 14, 2022
Uamuzi wa serikali ya Uingereza kufungia mali yake unalemaza shughuli za Klabu ya Soka ya Chelsea, kiungo muhimu cha utajiri wa Abramovich, na kutoa pigo lingine kubwa kwa biashara yake.
Takriban watoto 71 wameuawa na zaidi ya 100 kujeruhiwa nchini Ukraine tangu Rais wa Urusi Vladimir Putin kuanzisha vita Februari 24, afisa wa bunge la Ukraine alisema Alhamisi.
Washington na Kyiv kwa pamoja zimekanusha kuwepo kwa maabara zinazokusudiwa kuzalisha silaha za kibiolojia nchini humo.
Urusi na Ukraine zimekubaliana kusitisha mapigano kwa siku moja Jumatano katika maeneo ya uokoaji ili kuruhusu raia kutoroka mapigano.