Lissu awakataa Mawakili wa Serikali, “Mimi si mwenzao, mimi ni mshtakiwa wa uhaini”
Lissu alieleza kutoridhishwa kwake na namna Wakili wa Serikali alivyomtaja kama “mwenzetu”, akisisitiza kuwa hana uhusiano wowote na upande huo wa mashtaka.
Lissu alieleza kutoridhishwa kwake na namna Wakili wa Serikali alivyomtaja kama “mwenzetu”, akisisitiza kuwa hana uhusiano wowote na upande huo wa mashtaka.
Tukio hilo limetokea leo asubuhi, wakati Lissu alipofikishwa mahakamani kwa ajili ya kuendelea kuwasilisha hoja za kupinga uhalali wa hati ya mashtaka dhidi yake. Hoja hizo alianza kuziwasilisha jana, Septemba 15, 2025.
Kwa mujibu wa hati ya mashtaka, Lissu anatuhumiwa kwamba mnamo Aprili 3 alikusudia “kuchochea wananchi kuzuia uchaguzi mkuu wa mwaka 2025.” Hata hivyo, mwanasiasa huyo mashuhuri anasema kosa hilo haliingii kwenye wigo wa makosa ya uhaini kwa mujibu wa sheria za Tanzania.
“Kupata huruma unaponewa si kosa, lakini jambo muhimu zaidi ni kupata haki. Siwaombi Waheshimiwa Majaji mnipe haki kwa sababu ya huruma, bali kwa mujibu wa viapo vyenu na kwa mujibu wa sheria,”
Shauri hilo lilitajwa leo kwa ajili ya kuendelea na usikilizwaji wa hoja za pingamizi zilizowasilishwa na Lissu, ambapo upande wa Jamhuri ulikuwa unakamilisha uwasilishaji wake kabla ya Lissu, anayejitetea mwenyewe, kujibu hoja hizo.
Katika uwasilishaji wa hoja zake hii leo Lissu alitoa hoja nzito akieleza kuwepo kwa tofauti kubwa kati ya rekodi mbili za kesi zinazotoka kwenye Mahakama tofauti moja kutoka Mahakama ya Kisutu ambayo nakala yake alipelekewa gereani Ukonga na nyingine kutoka Mahakama Kuu ambayo aliipata jana akiwa mahakamani hapo.
Lissu alitoa kauli hiyo leo mbele ya Jopo la Majaji watatu wa Mahakama Kuu ya Tanzania Kanda ya Dar es Salaam, akifafanua kuwa uamuzi huo umetokana na uzito wa kesi hiyo, ambayo endapo atapatikana na hatia, adhabu yake ni kunyongwa hadi kufa.
Ikumbukwe Agosti 18, 2025, Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu ilibainisha kuwa kesi hiyo inakwenda Mahakama Kuu baada ya hatua za Kisheria kukamilika.
Makamu Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Tanzania Bara Stephen Wasira amesema kwamba kazi ya chama hicho kwa sasa ni kuisaka dola kwani mchakato wa kura za maoni zilishapita hivyo hakuna sababu ya kuwa na mgawanyiko tena.
“Najua kulikuwepo na maneno au vijineno eti utaratibu umekiukwa na mimi nililaumiwa kwa jinsi nilivyosema pale kwenye mkutano mkuu, lakini nasema waliokuwa wanasema hayo ama hawafahamu utaratibu wa chama chetu na kama wanafahamu labda wamesahau au wanajifanya hamnazo,” alisema Kikwete.