Mwenyekiti wa walimu wasio na ajira akamatwa
Mwenyekiti wa Umoja wa Walimu Wasio na Ajira Tanzania (NETO), Joseph Paulo Kaheza amekamatwa akiwa mkoani Geita kwa kile kinachodaiwa kuwa ni vuguvugu la kupigania ajira kwa walimu wa Tanzania.
Mwenyekiti wa Umoja wa Walimu Wasio na Ajira Tanzania (NETO), Joseph Paulo Kaheza amekamatwa akiwa mkoani Geita kwa kile kinachodaiwa kuwa ni vuguvugu la kupigania ajira kwa walimu wa Tanzania.
Mbunge wa Viti Maalum Esther Bulaya amesisitiza kuwa yeye bado ni mwanachama wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo(Chadema), isipokua suala la yeye kufukuzwa uanachama ni mambo ya ndani ya chama na ndio maana mpaka leo wanapigania haki yao ya kuwa wanachama wa Chadema.
Msemaji Mkuu wa serikali, Gerson Msigwa, amesema kuwa kuanzia mwaka huu, wanahabari nchini Tanzania watatolewa kadi za habari za kidijitali kama sehemu ya mpango wa serikali wa kuboresha sekta ya habari.
Rais wa Chama cha Mawakili Tanganyika (TLS), Boniface Mwabukusi leo Jumanne Februari 18, 2025, kwenye Uzinduzi wa kampeni ya Kitaifa ya msaada wa kisheria ya Mama Samia Jijini Mwanza, ameshauri kuzingatiwa kwa Ibara ya Tisa ya Katiba ya Tanzania yenye kuhimiza kuhusu utu, Upendo na utii kama suluhu ya migogoro mingi ya kijamii.
Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA), Plasduce Mbossa, amekanusha taarifa zinazosambaa mitandaoni kuwa Tanzania imesaini mkataba wa kuipa Kampuni ya Saudi-Africa Development Company (SADC) haki ya kuendesha Bandari ya Bagamoyo.
Ziara ya Rais Samia nchini Ethiopia imeanza leo ambapo anatarajia kuhitimisha Februari 16,2025.
Imeelezwa kuwa jumla ya madereva bodaboda 759 wamefariki dunia kutokana na ajali za barabarani kati ya mwaka 2022 na 2024.
Kundi la M23 linaloungwa mkono na Rwanda liliongeza mashambulizi yake siku ya Alhamisi kupitia mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) na linaonekana kuwa na nia ya kuchukua mji muhimu, huku Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Antonio Guterres, akitoa wito wa amani.
Katibu wa Jumuiya na Taasisi za Kiislam nchini Tanzania, Sheikh Issa Ponda, pamoja na viongozi wengine 11 wa Kiislam, ndio waliofungua kesi hiyo ya kikatiba katika Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam wakipinga mamlaka ya Baraza Kuu la Waislamu Tanzania (BAKWATA) juu ya maamuzi yanayohusu masuala ya dini.
Hii leo inatajwa kwa ajili ya kuangaliwa iwapo upelelezi wa kesi umekamilika, ingawa imefungwa mikono kuendelea na hatua zaidi baada ya Mkurugenzi wa Mashtaka nchini kuwasilisha kusudio la kukata rufaa katika Mahakama ya Rufani kupinga uamuzi wa Mahakama Kuu kuhusu kupatikana kwa dhamana ya mshtakiwa kutokana na kuangalia uhalali wa kesi ya jinai kwa haraka.