Bunge la Zambia Lapitisha Kwa Utata Muswada wa Kubadili Sheria za Uchaguzi
Muswada huo unapendekeza kurekebisha baadhi ya vifungu vya katiba ya taifa hilo lenye utajiri wa shaba kusini mwa Afrika, ikiwemo kuongeza idadi ya viti vya wabunge wanaochaguliwa pamoja na kutenga viti 40 kwa wanawake, vijana na watu wenye ulemavu. Aidha, muswada huo unapendekeza kuondoa kikomo cha mihula miwili ya miaka mitano kwa mameya.