Pele kusalia hospitalini kutokana na maambukizi ya njia ya mkojo

Pele mwenye umri wa miaka 81 alilazwa katika hospitali ya Albert Einstein mnamo Feb 13

0
Mchezaji kandanda, Pele

Nyota wa soka wa Brazil, Pele atasalia hospitalini kutokana na maambukizi ya njia ya mkojo katika hospitali ya Sao Paulo, ambako tayari alikuwa akipokea matibabu ya chemotherapy kwa uvimbe kwenye utumbo mpana, kituo hicho kilisema Jumatatu.

Mchezaji huyo wa zamani mwenye umri wa miaka 81 anayejulikana kama “O Rei” (The King) awali alilazwa katika hospitali ya Albert Einstein huko Sao Paulo mnamo Februari 13 kuendelea na matibabu yake ya uvimbe wa utumbo uliogunduliwa mnamo Septemba

Amelazwa hospitalini tangu wakati huo.

Siku nane baada ya kulazwa, hospitali hiyo ilisema iligundua maambukizi ya njia ya mkojo wakati wa uchunguzi wa kawaida.

 “Huenda akaruhusiwa kutoka hospitalini katika siku chache zijazo,” hospitali ilisema katika taarifa Jumatatu.

Pele alifanyiwa upasuaji wa uvimbe huo Septemba 4, akikaa mwezi mmoja hospitalini kabla ya kuruhusiwa kuendelea na matibabu ya kemikali.

Ni hivi punde zaidi katika msururu wa matatizo ya kiafya kwa nyota huyo, ambaye kuonekana kwake hadharani kumezidi kuwa nadra.

Akizingatiwa kuwa mwanasoka bora zaidi, Edson Arantes do Nascimento — jina halisi la Pele — ndiye mchezaji pekee katika historia kushinda vikombe vitatu vya Dunia (1958, 1962 na 1970).

Alijiunga na kandanda ya kimataifa akiwa na miaka 17 pekee kwa kufunga mabao ya kuvutia, yakiwemo mawili kwenye fainali dhidi ya wenyeji Sweden, Brazil iliposhinda Kombe la Dunia kwa mara ya kwanza mwaka wa 1958.

Aliendelea kufanya vyema katika kandanda ya kimataifa akifunga zaidi ya mabao 1,000 kabla ya kustaafu mwaka 1977. “Kama nilivyokuwa nikifanya kila mwezi, ninaenda hospitali kuendelea na matibabu,” Pele alisema kwenye mitandao yake ya kijamii mnamo Februari 13.

In this article

East Africa Premier News Source with Top Stories, Special Features and more.
Uncensored & Undaunted