DR Congo: Ajali ya treni yasabisha vifo vya watu 75

Watu husafiri kwa treni za mizigo kinyume cha sheria mara kwa mara kwa sababu ya ukosefu wa treni za abiria na ugumu wa kusafiri kwa barabara.

0

Idadi ya waliofariki katika ajali ya treni kusini mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo imefikia 75, maafisa walisema Jumapili, huku wataalam wakianza kuangalia sababu za ajali hiyo.

Maafisa Jumamosi walitoa idadi ya wanaume, wanawake na watoto 60 waliouawa katika ajali hiyo, iliyotokea Alhamisi usiku wakati treni ya mizigo ilipoacha njia.

Idadi mpya ya waliofariki ilitoka kwa Fabien Mutomb, mkuu wa kampuni ya reli ya serikali SNCC, baada ya kutembelea eneo hilo na wachunguzi wa ajali hiyo.

Kati ya watu 125 waliojeruhiwa 28 walikuwa katika hali mbaya, ilisema wizara ya mawasiliano.

Maafisa wa shirika la reli hawajasema kilichosababisha ajali hiyo, lakini wachunguzi watakuwa wakiangalia hali ya reli.

Waziri wa Mambo ya Ndani wa jimbo hilo, Deodat Kapenda, ambaye ni miongoni mwa waliotembelea eneo hilo, alisema katika taarifa yake Jumapili jioni kwamba ajali hiyo ilionekana kusababishwa na kupoteza kasi ya treni kwa ghafla.

Mutomb, katika taarifa yake, alisema sababu moja inaweza kuwa ni treni ilikuwa imebeba abiria wengi kupita kiasi.

“Hatua zitachukuliwa kuhakikisha kuwa tukio la aina hii halitokei tena,’ na waliohusika wataadhibiwa, aliongeza.

Kilichosababisha ajali

Siku ya Jumamosi, mkurugenzi wa miundombinu wa SNCC Marc Manyonga Ndambo aliiambia AFP treni hiyo ilikuwa imeundwa na mabehewa 15, 12 kati yao matupu.

Treni ilikuwa inatoka Luena katika jimbo jirani kuelekea mji Tenke mji wa uchimbaji madini, karibu na Kolwezi, ajali ilipotokea.

Treni iliacha njia saa 5:50 usiku (2150 GMT) siku ya Alhamisi katika kijiji cha Buyofwe, takriban kilomita 200 (maili 125) kutoka Kolwezi, mabehewa yake saba yakitumbukia kwenye maji.

Ilikuwa imebeba abiria wengi kupita kiasi wakati huo, alisema Manyonga Ndambo, akizungumza kwa njia ya simu kutoka Lubumbashi.

Watu husafiri kwa treni za mizigo kinyume cha sheria mara kwa mara kwa sababu ya ukosefu wa treni za abiria na ugumu wa kusafiri kwa barabara.

Treni kuacha njia yake ni jambo la kawaida nchini DRC, kama ilivyo  ajali za meli na boti zilizojaa kupita kiasi kwenye maziwa na mito ya nchi hiyo.

Kulingana na hifadhidata iliyodumishwa na AFP, ajali ya wiki jana ilikuwa mbaya zaidi duniani katika kipindi cha miaka miwili iliyopita, na ajali ya tatu kwa mbaya zaidi barani Afrika katika kipindi cha miaka10 iliyopita.

Ajali ya mwisho katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo ya aina hii ilitokea mwaka wa 2014, wakati treni nzuri ambayo mamia ya watu walikuwa wakisafiria kuacha njia katika eneo la Katongola, kusini mashariki mwa mkoa wa Kataga, na kuua watu 136.

Mutomb anatarajiwa kurejea Kinshasa siku ya Jumatatu kuripoti kuhusu uharibifu huo, wizara ya mawasiliano ilisema.

In this article

East Africa Premier News Source with Top Stories, Special Features and more.
Uncensored & Undaunted