Waziri Mkuu wa Australia atahadharisha ushiriki wa Rais Putin kwenye mkutano wa G20

Amesema tayari Marekani iko katika mwelekeo wa kuutaja uvamizi wa Ukraine kuwa uhalifu wa kivita. 

0

Waziri mkuu wa Australia Scott Morrison amesema hii leo kwamba mpango wa Rais Vladmir Putin wa Urusi wa kutaka kushiriki mkutano wa kilele wa kundi la nchi tajiri na zinazoinukia kiuchumi la G20 licha ya kushuhudiwa mgogoro wake na Ukraine, ni hatua ya kuvuka mpaka. 

Mkutano huo utafanyika baadae mwaka huu huko nchini Indonesia. Morrison amewaambia waandishi habari mjini Melbourne kwamba uvamizi wa Urusi nchini Ukraine ni hatua ya kimabavu na ukiukaji wa sheria ya kimataifa na kwa hivyo fikra ya kukaa kwenye meza moja na Putin ni hatua ya kuvuka mipaka. 

Amesema tayari Marekani iko katika mwelekeo wa kuutaja uvamizi wa Ukraine kuwa uhalifu wa kivita. 

Jana waziri wa mambo ya nje wa Marekani Antony Blinken alisema Marekani imebaini kwamba vikosi vya Urusi vimefanya uhalifu wa kivita ndani ya Ukraine akisema nchi hiyo iliwalenga makusudi raia na kutumia mbinu za kivita zilizoshuhudiwa Chechnya na Syria.

In this article

East Africa Premier News Source with Top Stories, Special Features and more.
Uncensored & Undaunted