Singapore yamhukumu kifo mtu mwenye ulemavu wa akili licha ya kilio kutoka kwa wanaharakati

Nagaenthran K. Dharmalingam alikamatwa mwaka wa 2009 kwa kusafirisha kiasi kidogo cha heroini, na alihukumiwa kifo mwaka uliofuata.

0
Wanaharakati wanashikilia mabango kupinga kunyongwa kwa Nagaenthran K. Dharmalingam, aliyehukumiwa kifo kwa kusafirisha heroini hadi Singapore, mnamo Machi 9. 2022. (Photo by Arif Kartono / AFP)

Mwanaume kutoka Malaysia mwenye ulemavu wa akili aliuawa nchini Singapore siku ya Jumatano, familia yake ilisema, baada ya kushindwa katika vita vya muda mrefu vya kisheria na licha ya watu wengi kutoka mataifa mengi kuoinga hukumu ya kifo dhidi yake na maombi ya kuhurumiwa.

Nagaenthran K. Dharmalingam alikamatwa mwaka wa 2009 kwa kusafirisha kiasi kidogo cha heroini katika jiji, ambalo lina baadhi ya sheria kali zaidi za madawa ya kulevya duniani, na alihukumiwa kifo mwaka uliofuata.

Mpango wa kumnyonga ulizua ukosoaji mkubwa kutokana na wasiwasi kuhusu ulemavu wake wa kiakili, Umoja wa Mataifa, Umoja wa Ulaya na bilionea wa Uingereza Richard Branson wakiwa miongoni mwa wale walioulaani.

Nagaenthran alitumia zaidi ya muongo mmoja akiweka wazi changamoto za kisheria lakini zilitupiliwa mbali na mahakama za Singapore, na rais wa jimbo hilo alikataa rufaa ya kumhurumia.

Kijana huyo mwenye umri wa miaka 34 aliuawa asubuhi, dada yake Sarmila Dharmalingam aliambia AFP.

“Haiwezekani kwamba Singapore iliendelea na hukumu ya kifo licha ya rufaa ya kimataifa ya kuokoa maisha yake,” alisema, akizungumza kutoka Malaysia.

Aliongeza kuwa familia ‘imehuzunishwa sana’ na “katika hali ya mshtuko.”

Reprieve, NGO inayoendesha kampeni dhidi ya hukumu ya kifo, ilisema Nagaenthran “alikuwa mwathiriwa wa upotovu mbaya wa haki.”

“Kunyongwa kwa mtu mlemavu wa akili, asiye na afya njema… ni jambo lisilowezekana na ni ukiukaji wa wazi wa sheria za kimataifa ambazo Singapore imechagua kusaini,” alisema mkurugenzi Maya Foa alisema.

Hapo awali Nagaenthran alipangiwa kunyongwa mwezi Novemba lakini hilo lilicheleweshwa huku akitaka kukata rufaa kwa misingi kwamba kumnyonga mtu mwenye ulemavu wa akili ni kinyume cha sheria za kimataifa.

Alikamatwa akiwa na umri wa miaka 21 alipojaribu kuingia Singapore akiwa na kifurushi cha heroini chenye uzani wa takriban gramu 43 – sawa na takriban vijiko vitatu.

Wafuasi wanasema ana IQ ya 69, kiwango kinachotambuliwa kama ulemavu, na alilazimishwa kufanya uhalifu.

Lakini mamlaka imetetea hukumu yake, ikisema maamuzi ya kisheria yaligundua kuwa alijua alichokuwa akifanya wakati wa kosa hilo.

Mamake aliwasilisha pingamizi la kisheria katika saa chache za mawisho Jumanne lakini lilikataliwa haraka na hakimu, na kusababisha jamaa zake kuangua kilio mahakamani.

Katika mahojiano na shirika la habari la AFP siku ya Jumanne, Branson alimtaka Rais wa Singapore Halimah Yacob kuonyesha huruma kwake Nagaenthran, akiitaja hukumu ya kifo kuwa ‘unyama.’

Singapore ilianza tena kutoa hukumu ya kifo mwezi uliopita baada ya kusimama kwa zaidi ya miaka miwili, ilipomnyonga mlanguzi mwingine wa dawa za kulevya.

Wanaharakati sasa wanahofia kuwa mamlaka yataanzisha wimbi la kunyongwa huku wafungwa wengine kadhaa waliohukumiwa kunyongwa hivi karibuni wakikata rufaa.

In this article

East Africa Premier News Source with Top Stories, Special Features and more.
Uncensored & Undaunted