Kenya: Kilio zaidi huku bei ya petroli, dizeli na mafuta taa ikipanda kwa Ksh.9 kwa lita

Mamlaka ya udhibiti wa nishati na petroli (EPRA) Jumanne ilitangaza kupanda kwa bei ya mafuta kwa KSh9 kwa lita.

0

Mamlaka ya udhibiti wa nishati na petroli (EPRA) Jumanne ilitangaza kupanda kwa bei ya mafuta kwa KSh9 kwa lita.

Mabadiliko ya bei yataanza kutumika kuanzia Juni 15 hadi Julai 14, 2022.

“Bei hizo ni pamoja na asilimia nane ya Kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT) kwa mujibu wa masharti ya Sheria ya Fedha ya 2018, Sheria ya Kodi ya 2020 na viwango vilivyorekebishwa kwa Ushuru wa Bidhaa uliorekebishwa kwa mfumuko wa bei kwa mujibu wa Notisi ya Kisheria namba 194/2020,” EPRA ilisema serikali itatumia Tozo ya Maendeleo ya Petroli (PDL) ili kuwaepusha wateja na bei hizo za juu.

Petroli ya Super itagharimu KSh159.12 kwa lita tofauti na KSh184.68 ambayo ingekuwa malipo kama PDL haingefunika tofauti ya KSh25.56.

Hii inamaanisha wamailiki wa magari watalipa KSh150 kwa lita

Kwa mafuta ya taa, serikali imepunguza bei kwa KSh42.43.

Bei hizo zitakuwa KSh127.94 kwa lita tofauti na KSh170.37 zilizokuwa awali.

Gharama ya petroli iliyoagizwa kutoka nje iliongezeka kwa asilimia 5.96 kutoka  $826.77 mwezi Aprili hadi $876.05  mwezi Mei.

Bei ya dizeli iliongezeka kwa asilimia 10.90 kutoka $899.36 mwezi Aprili hadi  $997.35 mwezi Mei.

Gharama ya mafuta ya taa hata hivyo imepungua kwa asilimia 0.34 kutoka $908.66 mwezi Aprili hadi $905.60 mwezi Mei.

Hii ndiyo bei ya juu zaidi ya mafuta katika historia ya Kenya.

Kupanda kwa bei ya mafuta kumekuwa mchangiaji mkuu wa kupanda kwa bei za bidhaa nchini katika mwaka uliopita.

Mnamo Mei, nchi ilitikiswa na wimbi la uhaba wa mafuta uliosababisha foleni ndefu kwenye vituo vya mafuta.

Hii ilisababishwa na mvutano kati ya wauzaji wakubwa wa mafuta na wapinzani wao wadogo juu ya usambazaji.

Hii ilileta pigo kwa wauzaji huru wa mafuta ambao kwa miaka mingi wamekuwa wakitegemea wauzaji wakubwa kwa usambazaji wa mafuta.

In this article

East Africa Premier News Source with Top Stories, Special Features and more.
Uncensored & Undaunted