Zelensky awasihi viongozi wa ulimwengu kushinikiza kumaliza vita kabla mwisho wa mwaka

Rais wa Ukraine Volodymyr Zelensky aliwataka viongozi wa G7 kufanya kila wawezalo kukomesha uvamizi wa Urusi katika nchi yake ifikapo mwisho wa mwaka.

0
Volodymyr Zelensky, rais wa Ukraine (Photo by Sergei SUPINSKY / AFP)

Rais wa Ukraine Volodymyr Zelensky siku ya Jumatatu aliwataka viongozi wa dunia waliokusanyika katika mkutano wa G7 kufanya kila wawezalo kukomesha uvamizi wa Urusi katika nchi yake ifikapo mwisho wa mwaka.

Katika hotuba yake kupitia video kwenye mkusanyiko wa viongozi katika Milima ya Alps ya Ujerumani, Zelensky alisema hali ya vita imefanya hali kuwa ngumu zaidi kwa wanajeshi wake.

Vita hivyo vinavyoonekana kuendelea hadi katika msimu wa baridi pia huenda vikaendelea kwa siku nyingi zaidi, alisema.

Kwa hivyo aliwataka viongozi wa G7 kufanya bidii kumaliza vita kufikia mwisho wa mwaka huu, ikiwa ni pamoja na kuzidisha vikwazo dhidi ya Urusi, chanzo kilisema.

Licha ya ahadi nyingi za kuadhibu Moscow ambazo washirika wa Magharibi wameanzisha, Zelensky aliwasihi “kutopunguza shinikizo na kuendelea kuiwekea Urusi vikwazo kwa wingi.”

In this article

East Africa Premier News Source with Top Stories, Special Features and more.
Uncensored & Undaunted