Mahakama ya Morocco yawafunga jela wahamiaji 33 wa Melilla

Takriban wahamiaji 23 walikufa baada ya takriban watu 2,000, wengi kutoka Sudan, kuvamia mpaka huo tarehe 24 Juni ikiwa ni idadi kubwa zaidi ya vifo kuwahi kutokea

0
Wahamiaji wakiwa na mabango wakati wa maandamano ya kupinga ubaguzi wa rangi katika mji mkuu wa Morocco Rabat mnamo Juni 28, 2022. (Photo by AFP)

Mahakama ya Morocco Jumanne iliwahukumu wahamiaji 33 kifungo cha miezi 11 jela kwa “kuingia nchini humo kinyume cha sheria,’ wakili wao alisema, baada ya jaribio baya la kuvuka mpaka katika eneo la Uhispania la Melilla mwezi uliopita.

Mahakama ya Nador, iliwahukumu “wahamiaji wote (33) kifungo cha miezi 11 jela kila mmoja,” Khalid Ameza aliiambia AFP, akielezea uamuzi huo kama “hukumu nzito sana.”

Takriban wahamiaji 23 walikufa baada ya takriban watu 2,000, wengi kutoka Sudan, kuvamia mpaka huo tarehe 24 Juni ikiwa ni idadi kubwa zaidi ya vifo kuwahi kutokea katika miaka ya kuvuka maeneo ya Ceuta na Melilla ya Uhispania, ambayo yanawakilisha mipaka pekee ya Umoja wa Ulaya na Afrika.

Wahamiaji hao 33 walifunguliwa mashitaka kwa ‘kuingia kinyume cha sheria katika ardhi ya Morocco,’ ‘unyanyasaji dhidi ya maafisa wa kutekeleza sheria,’ kushiriki katika ‘mkusanyiko wenye silaha’ na ‘kukataa kutii amri’ kulingana na taarifa ya mahakama.

“Tunatumai kuwa mahakama ya rufaa itarekebisha hukumu hii kali,” ofisi ya Nador ya shirika la haki za binadamu la AMDH ilisema.

Kesi tofauti, pia huko Nador, ya kundi la wahamiaji haramu iliyojumuisha mtoto mdogo iliyofunguliwa wiki iliyopita lakini imeahirishwa hadi Julai 27, mahakama ilisema.

Kundi hilo linashutumiwa kwa ‘kushiriki katika genge la uhalifu kwa nia ya kuandaa na kuwezesha’ uhamiaji usio wa kawaida, miongoni mwa mashtaka mengine.

Kundi la kutetea haki za Kihispania Caminando Fronteras linasema takriban watu 37 walipoteza maisha katika tukio la Juni 24.

Umoja wa Mataifa, Umoja wa Afrika na mashirika huru ya kutetea haki za binadamu yamelaani matumizi ya nguvu kupita kiasi yanayofanywa na maafisa wa usalama wa Morocco na Uhispania.

Shirika la kutetea haki za binadamu la CNDH linaloungwa mkono na serikali ya Morocco lilisema wiki iliyopita kwamba wale waliofariki huenda ‘walikosa hewa.’

CNDH ilitetea hatua za vikosi vya Morocco, ikisema visa vya unyanyasaji ‘vimetengwa’ na kutaja hatari inayoletwa na ‘idadi kubwa ya wahamiaji’ kubeba fimbo na mawe.

In this article

East Africa Premier News Source with Top Stories, Special Features and more.
Uncensored & Undaunted