Wanafunzi wa gradi ya 6 Kenya kuanza mtihani wao wa kitaifa juma lijalo

Zoezi hilo litashuhudia wanafunzi wapatao milioni 1.3 wakijiandaa kwa mitihani ya kitaifa inayotarajiwa kufanyika kuanzia Novemba 28 hadi 30.

0
Wanafunzi wakiwa darasani Kenya.

Siku ya Ijumaa tarehe 25, wanafunzi wa kwanza wa gradi ya 6 watafanya mazeozi kwa ajili ya mitihani mipya ya Tathmini ya Elimu ya Shule ya msingi ya Kenya (KPSEA), ambayo itachukua nafasi ya Cheti cha Elimu ya msingi ya Kenya (KCPE) chini ya ratiba mpya ya mtaala wa umilisi (CBC).

Zoezi hilo litashuhudia wanafunzi wapatao milioni 1.3 wakijiandaa kwa mitihani ya kitaifa inayotarajiwa kufanyika kuanzia Novemba 28 hadi 30.

Kisha wanafunzi hao watahitimu na kuendelea hadi darasa la 7 Januari, ambapo watajiunga na shule za Sekondari za Vijana chini ya mpango wa CBC.

Mitihani ya KCPE pia itafanywa tarehe sawa, kuruhusu wanafunzi wa darasa la 8 kukamilisha tathmini zao kwa kutumia mfumo wa 8-4-4.

Mpango mpya wa CBC unatumika kwa wanafunzi wa ngazi ya 6(Daraza la 6). Hii inamaanisha kuwa kutakuwa na makundi mawili ya watahiniwa wa KCPE kabla ya mpito kamili wa mtaala mpya.

KPSEA itaundwa kama ifuatavyo.

Masomo yatakayojaribiwa ni Hisabati, Kiingereza, Kiswahili, Sayansi Shirikishi(I.S) ambayo yanahusu Sayansi ya Nyumbani, Kilimo, Sayansi na Teknolojia na PHE.

Pia kutakuwa na Sayansi ya Ubunifu na Jamii (C.A.S.S) ambayo inajumuisha Sanaa na Ufundi, Muziki, Mafunzo ya Jamii na Elimu ya Dini.

Katika mtaala mpya, insha ya Kiswahili na Kingereza havitajaribiwa.

Muda uliotengewa kwa ajili ya masomo hayo ni Hisabati (saa1 dakika 20), Kiingereza na Kiswahili (saa 1), I.S na C.AS.S (saa 1 dakika 40).

Wanafunzi wwnye mahitaji maalum pekee ndio watakaopewa muda wa ziada.

Baada ya kukamilika kwa tathmini, karatasi hizo zitawasilishwa kwa afisi mahususi za elimu za kaunti ndogo na kukusanywa na wasimamizi wa vituo wakiwa na maafisa wa usalama.

Mchakato wa kusahihisha utakuwa wa kipekee kutoka kwa mifumo ya kitamaduni ya kusahihisha huku Baraza la kitaifa la mitihani nchini (KNEC) lilifichua kuwa KPSEA itatiwa alama kwa kutumia teknolojia mpya na walimu hawatahusika katika zoezi hilo.

Hii ni baada ya KNEC kupata Mashini za Optical Mark Recognition (OMR) zitakazofanya alama za tahmini ya darasa la sita kielektroniki.

Mshini huashiria kazi ya watahiniwa kwa kunasa karatasi zao za majibu kwa kutumia alama maalum. Mashini hizo zinasemekana kuweka alama katika bati za karatasi 1000 na 2000, hivyo kufanya mchakato huo kuchukua muda mfupi.

Alama za mwisho za KPSEA zitajumlishwa kutoka kwa tathmini za Msingi za shule (S.B.A) na Tathini Muhtasari wa kitaifa (S.N.A).

Takribana asilimia 60 ya alama za wanafunzi zitatoka katika S.B.A ambayo inajumuisha tathmini ambazo wamekuwa wakifanya kila mwaka katika madarasa ya msingi ya juu, Darasa la 4,5 na 6.

Hizi ni tathmini ambazo kwa kawaida hufanywa na walimu wa darasani, wakiongozwa na KNEC. Zinafanywa kwa njia ya Miradi, vitendo, mikoba na tathmini za simulizi.

Asilimia 40 iliyosalia ya alama za wanafunzi itatokana na tathmini za shule ya msingi inayojulikana kwa jina lingine kama mtihani wa KPSEA, ambao utakuwa katika mfumo wa maswali ya chaguo-nyingi.

Cheti cha mwisho cha CBC kitatolewa baada ya kukamilika kwa darasa la 12, ikilinganishwa na utoaji wa kitamaduni baada ya kumaliza mitihani ya KCPE.

Hati za matokeo zitatolewa na KNEC baada ya kukamika kwa uwekaji alama, ambayo itatangazwa tarehe ambayo haijathibitishwa.

In this article

East Africa Premier News Source with Top Stories, Special Features and more.
Uncensored & Undaunted