Mahakama Kuu ya Marekani kusikiliza kesi dhidi ya vitabu vya LGBTQ Mashuleni
Mahakama Kuu ya Marekani, ambayo ina wingi wa majaji wa mrengo wa kihafidhina, inatarajiwa kusikiliza kesi leo Jumanne kuhusu iwapo wazazi wana haki ya kidini kuwazuia watoto wao kuhudhuria madarasa yanayosoma au kujadili vitabu vyenye maudhui ya LGBTQ.