Tundu Lissu akataa Mahakama kumteulia Wakili, asema atajitetea mwenyewe kwenye Kesi ya Uhaini
Lissu alitoa kauli hiyo leo mbele ya Jopo la Majaji watatu wa Mahakama Kuu ya Tanzania Kanda ya Dar es Salaam, akifafanua kuwa uamuzi huo umetokana na uzito wa kesi hiyo, ambayo endapo atapatikana na hatia, adhabu yake ni kunyongwa hadi kufa.