DR. JOYCE KITHURE: EMPOWERING WOMEN IS NOT AN EVENT
“Empowering women is not an event; it is acontinuous commitment.” With these words,Dr.Joyce G. N. Kithure, Kenya’s Second Lady, opened…
“Empowering women is not an event; it is acontinuous commitment.” With these words,Dr.Joyce G. N. Kithure, Kenya’s Second Lady, opened…
This decision comes days after the European Parliament halts funding to Tanzania over political repression, Post-election crackdown with violence and killings, Internet shutdowns, abductions, and intimidation.
In a joint hard-hitting statement on Friday, December 5, the envyos also called on the Tanzanian government to urgently release all the bodies of those killed during the protests.
The review comes amid growing international scrutiny following the EU Parliament’s resolution calling for accountability and the release of political prisoners.
Meta Platform is facing growing criticism after disabling accounts belonging to prominent Tanzanian activist Mange Kimambi, and restricting access to others within Tanzania.
Uamuzi huo umetolewa leo Jumatano Disemba 3, 2025 na Hakimu Mkazi Mkuu, Aaron Lyamuya, baada wakili wa Serikali, Titus Aron kuileleza Mahakama hiyo kuwa Mkurugenzi wa Mashtaka nchini Tanzania( DPP) hana nia ya kuendelea na mashtaka shidi ya washtakiwa hao wawili.
The force that was used corresponds to the situation at hand. When we are told that we used excessive force in that incident… Were we supposed to simply watch that mob of demonstrators who were prepared to overthrow the government until they succeeded?
In the heart of Tana River County, a beacon of hope is shining bright. The ‘ALIVE’ programme, a partnership between…
Rais Samia Suluhu Hassan amesema sifa ya Tanzania kama kisiwa cha amani imeanza kuporomoka kutokana na matukio ya vurugu, uchochezi na matumizi ya dini katika siasa, akisisitiza kuwa vitendo hivyo vinadhoofisha misingi iliyoiweka nchi hiyo kwenye heshima ya kimataifa kwa miongo mingi.
Rais wa Tanzania Samia Suluhu Hassan amesema tofauti za kisiasa au mapenzi binafsi kwa kiongozi haziwezi kuwa sababu ya kuvuruga amani ya nchi, akisisitiza kuwa Tanzania imejengwa katika misingi ya demokrasia na utulivu tangu kuanzishwa kwake.
Akihutubia wazee wa Dar es Salaam leo, Rais Samia amesema kuwa Serikali ya Awamu ya Sita imeendelea kuboresha huduma za jamii na uchumi, na kwamba wanaoeneza chuki dhidi yake hawapaswi kutumia misingi ya dini au ukabila kuibua mgawanyiko.
“Hata kama aliyepo juu ya Serikali humtaki, kuna muda. Hii ni nchi ya kidemokrasia; huyu mtu ataongoza hadi kipindi hiki. Kama amefanya kosa, lisemeni kosa la kuongeza huduma bora za afya? Au kujenga mashule mazuri? Au kukuza uchumi hadi kusifiwa duniani? Kosa letu ni nini?” alihoji.
Ameongeza kuwa kutopenda kiongozi hakupaswi kuwa kichocheo cha vurugu: “Kama mtu hampendi anayeongoza, tustahimili tu. Ataongoza, ataondoka. Wote walioongoza tangu awamu ya kwanza, je, wote walipendwa? Kulikuwa na vurugu? Kama haumpendi Samia kwa sababu ya dini yake au alikotoka, hakuna sababu ya kuvuruga nchi.”
Rais Samia pia aliwaonya wananchi dhidi ya kile alichokiita “sumu za kisiasa” zinazoenezwa kwa jina la dini, akisema mbinu hizo hujenga chuki na kuharibu umoja wa taifa.
“Niwaombe sana: zile sumu zinazotiwa huko, mnapotiwa sumu tumieni akili zenu. Hakuna eneo baya la kumpata mtu kama dini; ukimlisha ubaya unajenga chuki moyoni. Wanasiasa wanamuharibu mtu kichwani,” alisema.
Katika wito mahsusi kwa viongozi wa dini, Rais Samia aliwahimiza kudumisha misingi ya maadili na kushikilia nafasi yao kama walinzi wa amani ambapo moja kwa moja alilitaja Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania(TEC), ambao mara kadhaa wamekuwa wakitoa waraka mzito dhidi ya mamlaka.Rais Samia alisema baraza hilo limekuwa likitoa matamko mara kwa mara, ikiwemo manane yaliyotolewa katika kipindi kifupi. Hata hivyo, amesema hata ndani ya TEC kuna viongozi wanaopinga matamko hayo wakiyaita batili, jambo analosema linaonesha kuwa msimamo huo si wa taasisi nzima.
“Viongozi wa dini kaeni kwenye mstari wenu. Dini zetu zote zinasema mamlaka yote yamewekwa na Mungu iwe mwanamke au mwanaume. Mungu ndiye anajua kwa nini Samia yupo hapa. Majoho yenu yaoneshe sura halisi. Hakuna kitabu cha dini kilichosema kitumie dini kuvuruga nchi,” alisisitiza.
Amehitimisha kwa kuwataka viongozi wa kidini na wananchi wote kulinda umoja wa kitaifa na kuepusha misuguano inayoweza kuhatarisha amani ya Tanzania.