ACT Wazalendo yamtaka Katambi kuachia mikutano ya hadhara
Mwenyekiti wa Chama cha ACT Wazalendo Taifa, Othman Masoud Othman, amemtaka Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Patrobas Katambi, kuacha hatua za kuzuia mikutano ya hadhara ya vyama vya siasa, akisema zinaenda kinyume na utamaduni na utaratibu wa muda mrefu wa kufanya siasa Zanzibar.