Chadema yadai Tundu Lissu yuko hatarini gerezani, yataka hatua za haraka
Katika taarifa kwa umma iliyotolewa leo Jumatatu, Julai 27, na kusainiwa na Mkurugenzi wa Mawasiliano na Uenezi wa chama hicho, Brenda Rupia, CHADEMA imesema imepokea taarifa kutoka kwa shirika la World Liberty Congress, linalojihusisha na masuala ya demokrasia, haki za binadamu na utawala wa sheria, zikieleza kuwepo kwa hofu kuhusu usalama wa Lissu.