Wakimbizi wa Congo wasimulia vifo na machafuko wakati vita vikianza upya
Maelfu wamekimbia huku raia wakijikuta tena katikati ya mapigano kati ya M23, jeshi la Congo na washirika wao.
Maelfu wamekimbia huku raia wakijikuta tena katikati ya mapigano kati ya M23, jeshi la Congo na washirika wao.
Uamuzi huo umetolewa leo Jumatano Disemba 3, 2025 na Hakimu Mkazi Mkuu, Aaron Lyamuya, baada wakili wa Serikali, Titus Aron kuileleza Mahakama hiyo kuwa Mkurugenzi wa Mashtaka nchini Tanzania( DPP) hana nia ya kuendelea na mashtaka shidi ya washtakiwa hao wawili.
Rais wa Tanzania Samia Suluhu Hassan amesema tofauti za kisiasa au mapenzi binafsi kwa kiongozi haziwezi kuwa sababu ya kuvuruga amani ya nchi, akisisitiza kuwa Tanzania imejengwa katika misingi ya demokrasia na utulivu tangu kuanzishwa kwake.
Akihutubia wazee wa Dar es Salaam leo, Rais Samia amesema kuwa Serikali ya Awamu ya Sita imeendelea kuboresha huduma za jamii na uchumi, na kwamba wanaoeneza chuki dhidi yake hawapaswi kutumia misingi ya dini au ukabila kuibua mgawanyiko.
“Hata kama aliyepo juu ya Serikali humtaki, kuna muda. Hii ni nchi ya kidemokrasia; huyu mtu ataongoza hadi kipindi hiki. Kama amefanya kosa, lisemeni kosa la kuongeza huduma bora za afya? Au kujenga mashule mazuri? Au kukuza uchumi hadi kusifiwa duniani? Kosa letu ni nini?” alihoji.
Ameongeza kuwa kutopenda kiongozi hakupaswi kuwa kichocheo cha vurugu: “Kama mtu hampendi anayeongoza, tustahimili tu. Ataongoza, ataondoka. Wote walioongoza tangu awamu ya kwanza, je, wote walipendwa? Kulikuwa na vurugu? Kama haumpendi Samia kwa sababu ya dini yake au alikotoka, hakuna sababu ya kuvuruga nchi.”
Rais Samia pia aliwaonya wananchi dhidi ya kile alichokiita “sumu za kisiasa” zinazoenezwa kwa jina la dini, akisema mbinu hizo hujenga chuki na kuharibu umoja wa taifa.
“Niwaombe sana: zile sumu zinazotiwa huko, mnapotiwa sumu tumieni akili zenu. Hakuna eneo baya la kumpata mtu kama dini; ukimlisha ubaya unajenga chuki moyoni. Wanasiasa wanamuharibu mtu kichwani,” alisema.
Katika wito mahsusi kwa viongozi wa dini, Rais Samia aliwahimiza kudumisha misingi ya maadili na kushikilia nafasi yao kama walinzi wa amani ambapo moja kwa moja alilitaja Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania(TEC), ambao mara kadhaa wamekuwa wakitoa waraka mzito dhidi ya mamlaka.Rais Samia alisema baraza hilo limekuwa likitoa matamko mara kwa mara, ikiwemo manane yaliyotolewa katika kipindi kifupi. Hata hivyo, amesema hata ndani ya TEC kuna viongozi wanaopinga matamko hayo wakiyaita batili, jambo analosema linaonesha kuwa msimamo huo si wa taasisi nzima.
“Viongozi wa dini kaeni kwenye mstari wenu. Dini zetu zote zinasema mamlaka yote yamewekwa na Mungu iwe mwanamke au mwanaume. Mungu ndiye anajua kwa nini Samia yupo hapa. Majoho yenu yaoneshe sura halisi. Hakuna kitabu cha dini kilichosema kitumie dini kuvuruga nchi,” alisisitiza.
Amehitimisha kwa kuwataka viongozi wa kidini na wananchi wote kulinda umoja wa kitaifa na kuepusha misuguano inayoweza kuhatarisha amani ya Tanzania.
Mwasilishaji wa ombi hilo, wakili Juan Carlos Gutierrez, anayewakilisha waathiriwa, anadai kwamba Rais Samia Suluhu Hassan, kama Amiri Jeshi Mkuu, anabeba jukumu la mwisho kwa madai hayo, akisema aliidhinisha moja kwa moja matumizi ya nguvu dhidi ya raia.
Serikali ya Tanzania imesema inafatilia kwa ukaribu makala mpya ya televisheni ya kimataifa ya CNN, ambayo imeeleza kwa kina madai ya ukiukwaji wa haki za binadamu na matukio ya vifo vya watu wakati wa maandamano yaliyofuatia uchaguzi wa Oktoba 29, 2025.
Makamu Mwenyekiti wa Chadema, John Heche, akitoa taarifa kwa vyombo vya habari leo Novemba 19, 2025, amesema Rais Samia hana mamlaka ya kimaadili wala kisiasa kuunda chombo cha kuchunguza kile chama hicho kinachokitaja kuwa ni uhalifu uliotekelezwa na Serikali yake dhidi ya raia waliokuwa wakidai haki zao za kidemokrasia.
Rais Samia amesema Tanzania kwa kiasi kikubwa bado inategemea mikopo kutoka taasisi za Kimataifa ili kuendeleza miradi yake ya maendeleo. Hata hivyo, kutokana na matukio yaliyotokea wakati na baada ya uchaguzi, huenda taasisi hizo zikapungukiwa na imani ya kuifadhili Tanzania. Ameeleza kuwa sasa ni muhimu kutafuta mbinu mbadala za kupata fedha, ikiwemo kutumia rasilimali za taifa zilizo ndani ya nchi.
Akitangaza hatua ya serikali kuunda Tume maalum ya uchunguzi, alisema uchunguzi huo utakuwa msingi wa kuelewa chanzo cha migogoro na kuchukua hatua za kurejesha maelewano ya kitaifa.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Mkurugenzi wa Sheria na Haki za Binadamu wa CHADEMA, Wakili Gaston Garubindi, maombi hayo yamesajiliwa na kupangwa mbele ya Jaji Obadia Bwegoge.
Taarifa ya Jeshi la Polisi imesema kuwa baadhi ya taarifa hizo zimeandaliwa kwa uangalifu ili kuzalisha taharuki, ikiwemo kuchukua matukio yaliyotokea katika nchi nyingine, kuyatengeneza upya, kisha kuyaunganisha na sauti za Kiswahili zenye lafudhi ya nchi yetu ili yaonekane yametokea nchini.