Tanzania yajitetea UNHRC, yakemea mataifa ya Magharibi kwa tathmini yenye upendeleo
Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imewasilisha msimamo wake mbele ya Baraza la Haki za Binadamu la Umoja wa…
Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imewasilisha msimamo wake mbele ya Baraza la Haki za Binadamu la Umoja wa…
Kwa mujibu wa taarifa hiyo, mafua makali ya Influenza na UVIKO-19 huambukizwa kupitia majimaji yanayotoka kwenye mfumo wa njia ya hewa ya mgonjwa, ambayo husambaa wakati wa kukohoa, kupiga chafya au kuzungumza.Vilevile, maambukizi yanaweza kutokea kwa kugusa mazingira yaliyochafuliwa na majimaji hayo.
WFP ilisema ilishambuliwa wiki iliyopita katika jimbo jirani la Upper Nile, eneo jingine linalochukuliwa kuwa ngome ya vikosi vya Machar.
Mwanzoni mwa Januari, Washington ilisimamisha msaada huo kwa Somalia kufuatia taarifa za wizi na kuingiliwa kwa shughuli za misaada na Serikali ya Somalia. Marekani ilidai kuwa maofisa wa Somalia walikamata kinyume cha sheria tani 76 za chakula cha msaada kilichokuwa kimetolewa kwa ajili ya raia waliokuwa katika mazingira magumu.
Kiongozi wa upinzani nchini Uganda, Bobi Wine, amesema yuko mafichoni kufuatia uchaguzi wa wiki iliyopita, huku kiongozi mwingine wa upinzani, Kizza Besigye, akiwa mahututi kutokana na hali mbaya ya afya, kwa mujibu wa mke wake.
Tundu Lissu ni mwanasiasa mkongwe wa upinzani na mmoja wa wakosoaji wakuu wa sera na utendaji wa serikali nchini Tanzania, anakabiliwa na mashtaka ya Uhaini ambayo anadaiwa kuyatenda mnamo mwezi Aprili 2025. Kesi yake imeibua mjadala mpana kuhusu uhuru wa kisiasa, nafasi ya upinzani na mwenendo wa haki katika masuala yanayogusa wanasiasa.
Zaidi ya watu milioni 20 wamejiandikisha kupiga kura katika nchi hiyo ya Afrika Mashariki, huku Museveni mwenye umri wa miaka 81 akitarajiwa kwa kiasi kikubwa kuendelea kutawala kwa muhula mwingine, akisaidiwa na udhibiti wake mkubwa wa vyombo vya dola na usalama baada ya zaidi ya miongo minne madarakani.
Maelfu wamekimbia huku raia wakijikuta tena katikati ya mapigano kati ya M23, jeshi la Congo na washirika wao.
Uamuzi huo umetolewa leo Jumatano Disemba 3, 2025 na Hakimu Mkazi Mkuu, Aaron Lyamuya, baada wakili wa Serikali, Titus Aron kuileleza Mahakama hiyo kuwa Mkurugenzi wa Mashtaka nchini Tanzania( DPP) hana nia ya kuendelea na mashtaka shidi ya washtakiwa hao wawili.
Rais wa Tanzania Samia Suluhu Hassan amesema tofauti za kisiasa au mapenzi binafsi kwa kiongozi haziwezi kuwa sababu ya kuvuruga amani ya nchi, akisisitiza kuwa Tanzania imejengwa katika misingi ya demokrasia na utulivu tangu kuanzishwa kwake.
Akihutubia wazee wa Dar es Salaam leo, Rais Samia amesema kuwa Serikali ya Awamu ya Sita imeendelea kuboresha huduma za jamii na uchumi, na kwamba wanaoeneza chuki dhidi yake hawapaswi kutumia misingi ya dini au ukabila kuibua mgawanyiko.
“Hata kama aliyepo juu ya Serikali humtaki, kuna muda. Hii ni nchi ya kidemokrasia; huyu mtu ataongoza hadi kipindi hiki. Kama amefanya kosa, lisemeni kosa la kuongeza huduma bora za afya? Au kujenga mashule mazuri? Au kukuza uchumi hadi kusifiwa duniani? Kosa letu ni nini?” alihoji.
Ameongeza kuwa kutopenda kiongozi hakupaswi kuwa kichocheo cha vurugu: “Kama mtu hampendi anayeongoza, tustahimili tu. Ataongoza, ataondoka. Wote walioongoza tangu awamu ya kwanza, je, wote walipendwa? Kulikuwa na vurugu? Kama haumpendi Samia kwa sababu ya dini yake au alikotoka, hakuna sababu ya kuvuruga nchi.”
Rais Samia pia aliwaonya wananchi dhidi ya kile alichokiita “sumu za kisiasa” zinazoenezwa kwa jina la dini, akisema mbinu hizo hujenga chuki na kuharibu umoja wa taifa.
“Niwaombe sana: zile sumu zinazotiwa huko, mnapotiwa sumu tumieni akili zenu. Hakuna eneo baya la kumpata mtu kama dini; ukimlisha ubaya unajenga chuki moyoni. Wanasiasa wanamuharibu mtu kichwani,” alisema.
Katika wito mahsusi kwa viongozi wa dini, Rais Samia aliwahimiza kudumisha misingi ya maadili na kushikilia nafasi yao kama walinzi wa amani ambapo moja kwa moja alilitaja Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania(TEC), ambao mara kadhaa wamekuwa wakitoa waraka mzito dhidi ya mamlaka.Rais Samia alisema baraza hilo limekuwa likitoa matamko mara kwa mara, ikiwemo manane yaliyotolewa katika kipindi kifupi. Hata hivyo, amesema hata ndani ya TEC kuna viongozi wanaopinga matamko hayo wakiyaita batili, jambo analosema linaonesha kuwa msimamo huo si wa taasisi nzima.
“Viongozi wa dini kaeni kwenye mstari wenu. Dini zetu zote zinasema mamlaka yote yamewekwa na Mungu iwe mwanamke au mwanaume. Mungu ndiye anajua kwa nini Samia yupo hapa. Majoho yenu yaoneshe sura halisi. Hakuna kitabu cha dini kilichosema kitumie dini kuvuruga nchi,” alisisitiza.
Amehitimisha kwa kuwataka viongozi wa kidini na wananchi wote kulinda umoja wa kitaifa na kuepusha misuguano inayoweza kuhatarisha amani ya Tanzania.