Mwenyekiti wa walimu wasio na ajira akamatwa
Mwenyekiti wa Umoja wa Walimu Wasio na Ajira Tanzania (NETO), Joseph Paulo Kaheza amekamatwa akiwa mkoani Geita kwa kile kinachodaiwa kuwa ni vuguvugu la kupigania ajira kwa walimu wa Tanzania.
Mwenyekiti wa Umoja wa Walimu Wasio na Ajira Tanzania (NETO), Joseph Paulo Kaheza amekamatwa akiwa mkoani Geita kwa kile kinachodaiwa kuwa ni vuguvugu la kupigania ajira kwa walimu wa Tanzania.
Mbunge wa Viti Maalum Esther Bulaya amesisitiza kuwa yeye bado ni mwanachama wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo(Chadema), isipokua suala la yeye kufukuzwa uanachama ni mambo ya ndani ya chama na ndio maana mpaka leo wanapigania haki yao ya kuwa wanachama wa Chadema.
Waziri Jane Ruth Aceng amesema kuwa wagonjwa hao wanane walikuwa wakitibiwa na sasa wamepona kikamilifu.
Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA), Plasduce Mbossa, amekanusha taarifa zinazosambaa mitandaoni kuwa Tanzania imesaini mkataba wa kuipa Kampuni ya Saudi-Africa Development Company (SADC) haki ya kuendesha Bandari ya Bagamoyo.
Ziara ya Rais Samia nchini Ethiopia imeanza leo ambapo anatarajia kuhitimisha Februari 16,2025.
Kiongozi wa upinzani wa Uganda, Kizza Besigye, anasema kuwa “anaumwa vibaya” gerezani siku tatu baada ya kuanza mgomo wa kula kupinga kizuizi chake, alieleza mmoja wa mawakili wake.
Umoja wa nchi 55 unakutana kuanzia Ijumaa katika mji mkuu wa Ethiopia, Addis Ababa, ambapo bara la Afrika linakutana na migogoro mikubwa inayoendelea katika DRC na Sudan, pamoja na kupunguzwa kwa msaada wa maendeleo kutoka kwa Rais wa Marekani Donald Trump, hatua inayolitesa bara hili kwa kiasi kikubwa.
Kundi la M23 linaloungwa mkono na Rwanda liliongeza mashambulizi yake siku ya Alhamisi kupitia mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) na linaonekana kuwa na nia ya kuchukua mji muhimu, huku Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Antonio Guterres, akitoa wito wa amani.
Afisa mkuu wa fedha wa Uganda, Lawrence Semakula, pamoja na wengine wanane, wamefunguliwa mashtaka ya udanganyifu na utakatishaji fedha kufuatia wizi wa karibu dola milioni 16 za Marekani zilizokuwa zimekusudiwa kulipia mikopo ya maendeleo, kulingana na nyaraka za mahakama.
Mapigano yaliyoibuka tena wiki iliyopita yalitokea katika majimbo ya South Kordofan na Blue Nile kati ya jeshi la Sudan na kundi la Sudan People’s Liberation Movement-North (SPLM-N) linaloongozwa na Abdel Aziz al-Hilu.