Siasa za visasi zadaiwa kukitafuna CHADEMA, G55 watangaza kujiondoa
Kundi la viongozi wa zamani wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), maarufu kama G55, limetangaza rasmi kujiondoa katika chama hicho kikuu cha upinzani nchini Tanzania, likidai kukithiri kwa ukiukwaji wa katiba, ubaguzi na siasa za visasi zinazoendeshwa na uongozi wa sasa.