Bei ya mafuta ya petroli, dizeli na mafuta ya taa yapungua nchini Tanzania
Taarifa ya Mkurugenzi Mkuu wa Ewura, Dk James Mwainyekule imeeleza kuwa bei za rejareja za mafuta ya petroli, dizeli na mafuta ya taa yaliyopokelewa kupitia Bandari ya Dar es Salaam zimepungua kwa shilingi 187 kwa lita, shilingi 284 kwa lita na shilingi 169 kwa lita mtawalia, ikilinganishwa na toleo la Machi Mosi mwaka huu.