Fujo,mabishano kwenye Kombe la Mataifa CAN huku Mali, Gambia na Ivory Coast zikishinda

Kulikuwa na matukio ya fujo kwenye michuano ya AFCON Mali ilipoifunga Tunisia katika mchezo uliokumbwa na mabishano

0
Mshambuliaji wa Tunisia, Wahbi Khazri (kushoto) akiwania mpira na kiungo wa Mali, Amadou Haidara wakati wa mechi ya Kundi F uwanjani Limbe Omnisport mjini Limbe (AFP)

Kulikuwa na matukio ya fujo kwenye michuano ya Kombe la Mataifa ya Afrika siku ya Jumatano Mali ilipoifunga Tunisia katika mchezo uliokumbwa na mabishano wakati mwamuzi alipopuliza kipenga cha mwisho kabla ya dakika 90 kutimia.

Tukio hilo lilitilia shaka kabisa ushindi wa Mali wa bao 1-0 dhidi ya mmoja wa washindi wa michuano hiyo mjini Limbe, huku Gambia na Ivory Coast nazo zikiibuka na ushindi wa bao moja huku awamu ya kwanza ya mechi za makundi kwenye kinyang’anyiro hicho ikikamilika.

Afisa wa Zambia, Janny Sikazwe aliashiria mwisho wa mechi hiyo huku saa ikionyesha dakika 89 na sekunde 42, na kuwaacha Tunisia wakiwa na hasira walipokuwa wakifuatilia mchezo dhidi ya wapinzani.

Huku hali ya sintofahamu ikitawala, Kocha wa Mali, Mohamed Magassouba, alikuwa akitoa taarifa kwa waandishi wa habari baada ya mechi kumalizika wakati ofisa mmoja alipoingia kwenye chumba chini ya stendi kuashiria kuwa mchezo huo ungeanza tena na kuwa dakika tatu zilikuwa zimesalia kabla mechi kukamilika.

Mali walirejea uwanjani lakini Watunisia hawakurudi na hivyo mwamuzi alifikisha mchezo kwenye tamati ya uhakika wakati Wamali hao walipoanza mchezo tena.

“Uamuzi wake hauelezeki. Sielewi jinsi alivyofanya uamuzi wake na tutaona kitakachotokea sasa,” kocha wa Tunisia Mondher Kebaier alisema kumhusu mwamuzi.

Hata hivyo, kukataa kwa timu hiyo ya Tunisia kurejea uwanjani kunaweza kuwaweka kwenye vikwazo zaidi kutoka kwa Shirikisho la Soka Afrika.

“Alipuliza kipenga kuashiria muda wa mchezo umeisha na akatuomba twende kwenye chumba cha kubadilishia nguo, kwa hivyo wachezaji walikuwa bafuni alipotuomba turudi nje,” Kebaier aliongeza.

“Katika miaka 30 katika mchezo huu sijawahi kuona kitu kama hicho.”

Mali bado waliweza kusherehekea ushindi wao, ambao walipata kwa mkwaju wa penalti wa Ibrahima Kone mara tu baada ya kipindi cha mapumziko kwenye mechi ya Kundi F.

Wahbi Khazri alipata nafasi ya kuisawazishia Tunisia katika robo ya mwisho ya mchezo huo lakini mkwaju wake wa penalti upande wa pili ukaokolewa na kipa wa Mali Ibrahim Mounkoro.

Mali ilimpatia mchezaji wa akiba El-Bilal Toure aliyetolewa kwa kadi nyekundu kabla ya matukio ya fujo kutokea katika uwanja wa Limbe.

Michezo inachezwa katika mji huo licha ya machafuko ya watu wanaotaka kujitenga katika eneo hilo.

Mshambuliaji wa Tunisia, Wahbi Khazri (kushoto) akiwania mpira na kiungo wa Mali, Amadou Haidara wakati wa mechi ya Kundi F uwanjani Limbe Omnisport mjini Limbe (AFP)

In this article

East Africa Premier News Source with Top Stories, Special Features and more.
Uncensored & Undaunted