Rais wa Senegal atangaza sikukuu ya kitaifa kusherehekea ushindi wa Kombe la AFCON

Ikiongozwa na nyota wa Liverpool, Sadio Mane, Senegal iliishinda Misri kwa mabao 4-2 katika mikwaju ya penalti

0
Mashabiki wa Senegal wakisheherekea ushindi wa timu yao katika kombe la AFCON mjini Dakar (Photo by CARMEN ABD ALI / AFP)

Rais wa Senegal Macky Sall ametangaza Jumatatu kuwa likizo ya kitaifa kusherehekea taji la kwanza kabisa la timu ya taifa ya Kombe la Mataifa ya Afrika kufuatia ushindi wao dhidi ya Misri, kituo cha Televesheni kilisema.

Sall, ambaye alipaswa kuzuru Comoro baada ya kuzuru Misri na Ethiopia, alighairi mkondo wa mwisho ili kuwakaribisha Simba wa Teranga watakaporejea Dakar saa 1300 GMT Jumatatu, RTS ilisema.

Ikiongozwa na nyota wa Liverpool, Sadio Mane, Senegal iliishinda Misri kwa mabao 4-2 katika mikwaju ya penalti Jumapili kwenye fainali huko Cameroon.

Mchezo huo ulikuwa umeisha bila bao baada ya muda wa ziada. Baada ya kushindwa mara mbili katika fainali za awali mwaka wa 2002 na 2019, Senegal hatimaye ilitwaa taji lao la kwanza la Kombe la Mataifa ya Afrika.

Simba watatuzwa na Sall siku ya Jumanne katika ikulu ya Dakar, televisheni ya RTS ilisema.

“Rais alitangaza Jumatatu kuwa sikukuu ya kitaifa, siku ya mapumziko ya kulipwa, kufuatia ushindi mkubwa wa Simba,” RTS ilisema, ikitoa amri ya rais.

In this article

East Africa Premier News Source with Top Stories, Special Features and more.
Uncensored & Undaunted