Kimbunga Emnati kimesababisha vifo vya watu wanne nchini Madagascar

Madagascar hukabiliwa na dhoruba nyingi na vimbunga kati ya Novemba na Aprili kila mwaka.

0

Takriban watu wanne wamefariki na makumi ya maelfu kuathiriwa baada ya Kimbunga Emnati kushambulia kisiwa cha Madagascar, maafisa walisema Ijumaa.

Madagascar bado inayumba kutokana na kimbunga kingine kilichogonga kisiwa hicho mapema mwezi huu, Emnati iliikumba Madagascar mwanzoni mwa juma, ikibeba upepo wa hadi kilomita 140 kwa saa.

“Kumekuwa na vifo vinne huko Farafangana” mji wa pwani kusini mashariki, kulingana na idadi ya awali ya Ofisi ya Kitaifa ya Kudhibiti Hatari ya Madagascar.

Takriban watu 72,200 wameathiriwa na kimbunga hicho, ambacho pia kilisababisha kukatika kwa barabara na daraja.

Moja ya nchi maskini zaidi duniani, Madagascar inakabiliwa na dhoruba nyingi na vimbunga kati ya Novemba na Aprili kila mwaka.

Dhoruba nyingine, Kimbunga Batsirai, kilipiga kisiwa hicho mnamo Februari 5, na kuathiri watu wapatao 270,000 na wengine 121 kufariki.

Dhoruba ya Tropiki Ana pia ilipiga mwishoni mwa Januari, na kuua takriban watu 100 huko Madagascar, Msumbiji, Malawi na Zimbabwe.

Eneo la kusini mwa Madagascar pia limekumbwa na ukame, na kusababisha utapiamlo kati ya wakazi.

In this article

East Africa Premier News Source with Top Stories, Special Features and more.
Uncensored & Undaunted