Msanii wa Nigeria Davido ashirikishwa katika wimbo rasmi wa Kombe la Dunia Qatar 2022

Onyesho la kwanza la wimbo huo litafanyika usiku wa leo kabla ya droo ya makundi inayotarajiwa kuanza saa 19:00 kwa saa za Qatar.

0

Mwimbaji wa Nigeria, David Adeleke, maarufu Davido, ameshirikishwa katika wimbo rasmi wa Kombe la Dunia la Qatar 2022.

Davido alitangaza hayo kwenye mtandao wake wa kijamii Ijumaa, akisema wimbo rasmi unaitwa “Hayya Hayya” (Better Together).

Aliandika kwenye Twitter, “Nimejivunia kushirikishwa kwenye Wimbo Rasmi wa #FIFAWorldCup 2022! Tuonane baadaye jioni ya leo. Hii ni ya Afrika! TULE!!!! WE RISE!

Kando na Davido, wimbo huo ulishirikisha nyota wa Marekani Trinidad Cardona, na nyota wa Qatar Aisha, wasanii watatumbuiza mashabiki na wimbo huo kabla ya droo ya mwisho ya michuano hiyo kutangazwa baadae leo jioni.

Wakizungumzia chaguo la Davido na wengine, FIFA kwenye ukurasa wake rasmi, ilisema chaguo lao “lililenga kuwaleta pamoja mashabiki wa kandanda kutoka ulimwenguni kote kupitia soka.”

“Mkakati wa burudani ulibuniwa ili kuunda uhusiano wa kiubunifu na wa maana kati ya mashabiki wa soka, wapenda muziki, wachezaji, wasanii, na mchezo wa soka na nyimbo wanazopenda wote.

“Kuwaleta pamoja nyota wa Marekani Trinidad Cardona, nyota wa Afrobeats Davido na mrembo kutoka Qatar Aisha unavuta hisia za Kombe la Dunia la FIFA™ na mkakati wa FIFA kwa kuleta pamoja msukumo kutoka duniani kote.”

Akizungumzia wimbo huo, Ofisi ya Mkuu wa Biashara ya FIFA, Kay Madati, alisema, “Kwa kuleta pamoja msanii kutoka Amerika, Afrika, na Mashariki ya Kati, wimbo huu unaashiria jinsi muziki – na soka – unavyoweza kuunganisha ulimwengu.

Onyesho la kwanza la wimbo huo litafanyika usiku wa leo mbele ya hadhira ya mashabiki wa soka duniani kote, ambao watajitokeza kutoka duniani kote kufuatilia droo inayotarajiwa kuanza saa 19:00 kwa saa za huko, FIFA ilisema.

In this article

East Africa Premier News Source with Top Stories, Special Features and more.
Uncensored & Undaunted