Elon Musk asema mpango wa kununua Twitter ‘umesitishwa kwa muda’

Tangazo la Ijumaa lilisababisha hisa za Twitter kushuka kwa asilimia 20

0
Elon Musk mmiliki wa Tesla na SpaceX

Elon Musk asema Ijumaa alikuwa anasimamisha kwa muda mpango wake wa kununua Twitter. Tangazo lake lilifanya bei za hisa za kampuni hiyo kushuka kwa kiasi kikubwa.

Musk, mtu tajiri zaidi duniani na mwanzilishi wa kampuni ya kutengeneza magari ya Tesla, alikuwa amefanya mabadiliko makubwa ya teknolojia katika mtandao huwa kuwa moja ya sehemu kuu za pendekezo lake la kunyakua Twitter kwa dola bilioni 44.

Wakati mpango huo ulipotangazwa mwishoni mwa mwezi wa Aprili alisema alitaka kuifanya Twitter kuwa ‘bora zaidi kuliko hapo awali.’

Takwimu za kuaminika za idadi ya watumiaji zinaonekana kuwa muhimu ili kutathmini vyanzo vya mapato vya siku zijazo.

“Mkataba wa Twitter umesitishwa kwa muda ukisubiri maelezo yanayounga mkono hesabu kwamba akaunti bandia zinawakilisha chini ya 5% ya watumiaji,” aliandika kwenye Twitter.

Ripoti hiyo  lilisema ukaguzi wa ndani ulihitimisha kuwa Twitter ilikuwa na ‘watumiaji wa kila siku wanaofadika kwa fedha’ milioni 229 katika robo ya kwanza ya mwaka huu, na ni asilimia tano tu iliyochukuliwa kuwa akaunti za uwongo au bandia.

Mchambuzi Dan Ives kutoka Wedbush alisema ‘onyesho la sarakasi’ la Twitter huenda likatafsiriwa kuwa ‘onyesho la kutisha watu la Friday the 13th.”

Wawekezaji wa Wall Street wana uwezekano wa kutafsiri tweet kama jaribio la Musk kujiondoa kwenye mpango huo au kujaribu kulazimisha bei ya chini ya hisa zake,” alisema Ives.

Ununuzi wa Twitter na Musk siku zote ulikusudiwa kuwa mgumu, na sasa unaweza kwenda visivyo,” mchambuzi wa soko Susannah Streeter wa Hargreaves Landsdown alisema.

Tangazo la Ijumaa lilisababisha hisa za Twitter kushuka kwa asilimia 20  kabla ya Wall Street kufunguliwa, lakini hisa za Tesla zilikuwa zinaongezeka.

Musk ni bosi wa Tesla na SpaceX na anakadiriwa kuwa na thamani ya dola bilioni 240, kulingana na Forbes.

Lakini mtindo wake wa umiliki mara kwa mara umemfanya aingie kwenye matatizo na mamlaka.

In this article

East Africa Premier News Source with Top Stories, Special Features and more.
Uncensored & Undaunted