Kenya yaandikisha idadi ndogo ya vijana katika kura za mwezi Agosti

Idadi ya wapiga kura vijana waliojiandikisha katika uchaguzi wa Agosti nchini Kenya imepungua tangu uchaguzi uliopita miaka mitano iliyopita, tume ya uchaguzi IEBC

0
Wafula Chebukati, mwenyekiti wa IEBC

Idadi ya wapiga kura vijana waliojiandikisha katika uchaguzi wa Agosti nchini Kenya imepungua tangu uchaguzi uliopita miaka mitano iliyopita, tume ya uchaguzi ilitangaza Jumatatu, ikionyesha kutojali miongoni mwa vijana waliokata tamaa kutokana na matatizo ya kiuchumi na ufisadi ulioenea.

Hii ni licha ya jumla ya watu waliojiandikisha kupiga kura kuongezeka kwa zaidi ya asilimia 12, Tume Huru ya Uchaguzi na Mipaka (IEBC) ilisema baada ya ukaguzi wa sajili ya wapigakura.

Kutakuwa na wapiga kura milioni 22.1 kwenye daftari — mara nyingi huonekana kama sehemu muhimu ambapo uchaguzi unaweza kuibiwa — kutoka milioni 19.6 miaka mitano iliyopita.

“Idadi ya vijana waliojiandikisha kupiga kura mwaka wa 2022 imefikia asilimia 39.84 ikiwa imepungua kwa asilimia 5.27 tofauti na mwaka 2017,” mwenyekiti wa IEBC Wafula Chebukati alisema.

Vijana wenye umri wa chini ya miaka 35 ni robo tatu ya waKenya wapatao milioni 50, kulingana na takwimu za serikali.

Wanawake ‘bado walikuwa na uwakilishi mdogo’ katika sajili ya wapigakura huku idadi ya wanawake waliojisajili ikiwa asilimia 49 ya jumla, Chebukati alisema.

Kenya itafanya uchaguzi wa rais na wabunge Agosti 9, chini ya kivuli cha chaguzi zilizopita ambazo mara nyingi zimekumbwa na ghasia za kikabila.

Ikiwa na idadi tofauti ya watu na makundi makubwa ya wapiga kura, Kenya kwa muda mrefu imekuwa ikikumbwa na ghasia za kijamii zilizochochewa kisiasa wakati wa uchaguzi, hasa baada ya kura ya maoni ya 2007 ambapo zaidi ya watu 1,100 walikufa.

Wapiga kura wengi vijana wanaonyesha kuwa hawana hamu ya kushiriki uchaguzi mwaka huu, wakiwa wamekatishwa tamaa na wanasiasa wengi ambao wanaoonekana kuwa wazembe na wafisadi.

Wakati wa ukaguzi huo, zaidi ya wapiga kura 246,000 waliofariki waliondolewa kwenye orodha ya wapiga kura, IEBC ilisema.

Chebukati alisema tume hiyo ilikuwa ikitoa takwimu hizo “katika hali ya uwazi na imejitolea kuwajaibikia wapiga kura.”

Kinyang’anyiro cha urais mwaka huu kinaelekea kuwa kati ya wagombea wawili kati ya Naibu Rais William Ruto, 55, na Raila Odinga, 77, mwanasiasa mkongwe na waziri mkuu wa zamani.

Wagombea wengine wawili wameidhinishwa kushiriki kinyang’anyiro cha kumrithi Rais Uhuru Kenyatta, ambaye lazima astaafu baada ya kuhudumu kwa mihula miwili ya miaka mitano mitano.

Ruto awali alipakwa mafuta na Kenyatta kuwa mrithi wake lakini amejikuta pekee yake baada ya Kenyatta na Odinga kuunda muungano mwaka wa 2018. Ruto anatumai safari yake ya kutoka kwa mchuuzi wa mitaani hadi mwanasiasa wa cheo cha juu itawavutia vijana wa Kenya, akijifanya msemaji wa “hustlers” wanaojaribu kupata riziki katika nchi inayotawaliwa na “dynasties.”

Familia za Kenyatta na Odinga zimetawala siasa za Kenya tangu uhuru mwaka 1963.

In this article

East Africa Premier News Source with Top Stories, Special Features and more.
Uncensored & Undaunted