Mwanawe Fela Kuti aghairi tamasha la Morocco kutokana na vifo vya wahamiaji

Mwimbaji na mcheza saxophone huyo alikuwa amepangwa kucheza siku ya Jumamosi katika tamasha la Jazzablanca katika jiji la bandari la Morocco la Casablanca.

0
Katika picha hii iliyopigwa Julai 18, 2018 mwanamuziki wa Nigeria Seun Kuti atumbuiza jukwaani wakati wa Tamasha la Nice la Jazz mjini Nice, kusini mashariki mwa Ufaransa.. – (Photo by VALERY HACHE / AFP)

Seun Kuti, mwanawe nguli wa muziki wa Afrobeat Fela Kuti, ameghairi tamasha nchini Morocco ili kuomboleza msiba wa wiki iliyopita kwenye mpaka wa eneo la Melilla nchini Uhispania ambapo takriban wahamiaji 23 wa Kiafrika walikufa.

Mwimbaji na mcheza saxophone huyo alikuwa amepangwa kucheza siku ya Jumamosi katika tamasha la Jazzablanca katika jiji la bandari la Morocco la Casablanca.

Lakini katika video aliyotuma kwenye Instagram, alitangaza “kwa masikitiko makubwa” kwamba yeye na bendi yake hawatahudhuria.

“Inaniuma kusema kwamba roho yangu imevunjika kabisa na matukio ya Ijumaa iliyopita,” alisema.

“Haiwezekani kwa nia njema na dhamiri njema kupanda jukwaani na kusherehekea na kuwa na wakati mzuri wakati Waafrika wengi wamepoteza maisha. Inabidi mtu awaomboleze.”

Tukio la Ijumaa lilikuwa baya zaidi katika miaka ya majaribio ya wahamiaji, kuvuka mpaka wenye ngome nyingi, moja ya mipaka ya pekee ya EU na Afrika.

Umoja wa Mataifa umeshutumu mamlaka za Morocco na Uhispania kwa kutumia “nguvu kupita kiasi” dhidi ya wahamiaji, na kutaka uchunguzi ufanyike.

Vyombo vya habari vya Uhispania na video mtandaoni zilionyesha watu wakiwa chini, wengine mikono yao ikiwa na damu na nguo zilizochanika.

Jazzablanca iliithibitishia AFP kwamba tamasha la Kuti lilikatishwa kutokana na ‘uamuzi wa kibinafsi wa msanii.”

Gwiji wa muziki wa jazz wa Ethiopia Mulatu Astatke, mwimbaji-mtunzi wa nyimbo na mwanasiasa wa Brazil Gilberto Gil na msanii wa muziki wa rock wa Israeli Asaf Avidan bado wako kwenye programu.

In this article

East Africa Premier News Source with Top Stories, Special Features and more.
Uncensored & Undaunted