Kampuni ya Kitanzania ilihamisha pesa kabla ya benki ya SVB kuporomoka

Kampuni za Kiafrika zinafuatilia kwa karibu kuona nini kitatokea baada ya kuporomoka kwa Benki ya Silicon Valley

0

Kampuni za Kiafrika zinafuatilia kwa karibu kuona nini kitatokea baada ya kuporomoka kwa Benki ya Silicon Valley yenye makao yake makuu nchini Marekani (SVB).

Benki hiyo iliyobobea katika kutoa mikopo kwa makampuni ya teknolojia, ilifungwa na wadhibiti ambao walitwaa mali yake siku ya Ijumaa.

Hata hiyo ilifikiwa baada ya SVB kuhangaika kutafuta pesa za kuzuia hasara kutokana na mauzo ya mali iliyoathiriwa na viwango vya juu vya riba.

Benki hiyo ilikuwa mshirika na kampuni iliyoanzisha kampuni ya Y Combinator, ambayo inasemekana ina zaidi ya kampuni changa 80 za Kiafrika katika jalada lake.

Rais wa Y-Combinator Garry Tan aliandika: “30% ya kampuni za YC zilizofichuliwa kupitia SVB haziwezi kufanya malipo katika siku 30 zijazo.”

Mwanzilishi wa Tanzania fintech NALA, Benjamin Fernandes, aliiambia Kipindi cha Redio cha BBC Focus on Africa kwamba walikuwa na benki na SVB.

“Nilipigiwa simu na mmoja wa wawekezaji wetu akisema tutoe pesa kwani benki hii itaanguka

Mara moja tulituma pesa hizo kwenye akaunti nyingine ya benki ambayo tunafanya nayo kazi.”

“Sidhani kama waanzishaji wengi wa wa kampuni za Kiafrika waliathiriwa ikilinganishwa na kile tulichofikiria mwanzoni kwa sababu sio benki nyingi zinazoanza na SVB. Kampuni ya Kiafrika inayoinukia ni vigumu kupata akaunti ya benki ya Marekani,” alisema.

In this article

East Africa Premier News Source with Top Stories, Special Features and more.
Uncensored & Undaunted