Waziri wa Uganda Agnes Nandutu ashtakiwa kwa kashfa ya ufisadi

Uchunguzi wa ufisadi dhidi ya mawaziri ni nadra nchini Uganda

0
Waziri Agnes Nandutu akiwasili katika Mahakama ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa kujibu mashitaka yanayohusiana na utakatishaji wa mabati ya Karamoja

Waziri wa Jimbo la Uganda anayehusika na Masuala ya Karamoja, Bi Agnes Nandutu alishtakiwa Jumatano kwa ufisadi katika kashfa inayoongezeka ya serikali kuhusu madai ya wizi wa maelfu ya mabati yaliyokusudiwa kwa mpango wa kutoa msaada katika eneo la kaskazini mashariki mwa Karamoja.

Siku ya Jumatano Agness Nandutu alizuiliwa gerezani na hakimu wa Kampala baada ya kukana hatia ya “kushughulikia mali inayoshukiwa,” kulingana na karatasi za mahakama.

Nandutu alituhumiwa kupokea mabati 2,000 kutoka kwa maduka ya serikali “ambayo alikuwa na sababu ya kuamini kuwa yalipatikana kutokana na upotevu wa mali ya umma.”

Tayari waendesha mashtaka wamewashtaki wabunge wengine wawili katika kesi hiyo hiyo, akiwemo waziri mdogo wa fedha wa Uganda. Mpango huo wa kutoa msaada unaendeshwa na ofisi ya waziri mkuu.

Mwendesha mashtaka mkuu nchini humo, Jane Frances Abodo, aliambia kituo cha redio nchini humo ofisi yake imefungua uchunguzi sambamba na maafisa wengine kadhaa, akiwemo makamu wa rais.

Uchunguzi wa ufisadi dhidi ya mawaziri ni nadra nchini Uganda.

In this article

East Africa Premier News Source with Top Stories, Special Features and more.
Uncensored & Undaunted