Mahakama Kutoa Uamuzi Mdogo Mapingamizi Ya Lissu Februari 11
Tundu Lissu alisisitiza kuwa kizimba kilichotumika hakiwezi kutambuliwa kama kizimba cha mashahidi kwa mujibu wa kanuni na tafsiri ya kisheria. Alidai kuwa kizimba hicho hakionekani na waheshimiwa majaji, hali ambayo kwa mtazamo wake inakiuka misingi ya usikilizwaji wa haki.