Shahidi wa Kificho Asema Ana Hofu Kutoa Ushahidi Hadharani Katika Kesi ya Uhaini ya Lissu
Shahidi wa kificho katika kesi ya uhaini inayomkabili Mwenyekiti wa CHADEMA, Tundu Lissu, ameieleza Mahakama Kuu kuwa ana hofu ya kutoa ushahidi wake hadharani, akisema suala hilo ni “very sensitive” na kwamba wafuasi wa chama hicho wanaweza kuwa na hasira naye licha ya kuwa na mahusiano mazuri na Viongozi wakuu wa Chadema.