U.S. Announces Full Review of Bilateral Ties With Tanzania Over Rights Violations
The review comes amid growing international scrutiny following the EU Parliament’s resolution calling for accountability and the release of political prisoners.
The review comes amid growing international scrutiny following the EU Parliament’s resolution calling for accountability and the release of political prisoners.
Rais wa Tanzania Samia Suluhu Hassan amesema tofauti za kisiasa au mapenzi binafsi kwa kiongozi haziwezi kuwa sababu ya kuvuruga amani ya nchi, akisisitiza kuwa Tanzania imejengwa katika misingi ya demokrasia na utulivu tangu kuanzishwa kwake.
Akihutubia wazee wa Dar es Salaam leo, Rais Samia amesema kuwa Serikali ya Awamu ya Sita imeendelea kuboresha huduma za jamii na uchumi, na kwamba wanaoeneza chuki dhidi yake hawapaswi kutumia misingi ya dini au ukabila kuibua mgawanyiko.
“Hata kama aliyepo juu ya Serikali humtaki, kuna muda. Hii ni nchi ya kidemokrasia; huyu mtu ataongoza hadi kipindi hiki. Kama amefanya kosa, lisemeni kosa la kuongeza huduma bora za afya? Au kujenga mashule mazuri? Au kukuza uchumi hadi kusifiwa duniani? Kosa letu ni nini?” alihoji.
Ameongeza kuwa kutopenda kiongozi hakupaswi kuwa kichocheo cha vurugu: “Kama mtu hampendi anayeongoza, tustahimili tu. Ataongoza, ataondoka. Wote walioongoza tangu awamu ya kwanza, je, wote walipendwa? Kulikuwa na vurugu? Kama haumpendi Samia kwa sababu ya dini yake au alikotoka, hakuna sababu ya kuvuruga nchi.”
Rais Samia pia aliwaonya wananchi dhidi ya kile alichokiita “sumu za kisiasa” zinazoenezwa kwa jina la dini, akisema mbinu hizo hujenga chuki na kuharibu umoja wa taifa.
“Niwaombe sana: zile sumu zinazotiwa huko, mnapotiwa sumu tumieni akili zenu. Hakuna eneo baya la kumpata mtu kama dini; ukimlisha ubaya unajenga chuki moyoni. Wanasiasa wanamuharibu mtu kichwani,” alisema.
Katika wito mahsusi kwa viongozi wa dini, Rais Samia aliwahimiza kudumisha misingi ya maadili na kushikilia nafasi yao kama walinzi wa amani ambapo moja kwa moja alilitaja Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania(TEC), ambao mara kadhaa wamekuwa wakitoa waraka mzito dhidi ya mamlaka.Rais Samia alisema baraza hilo limekuwa likitoa matamko mara kwa mara, ikiwemo manane yaliyotolewa katika kipindi kifupi. Hata hivyo, amesema hata ndani ya TEC kuna viongozi wanaopinga matamko hayo wakiyaita batili, jambo analosema linaonesha kuwa msimamo huo si wa taasisi nzima.
“Viongozi wa dini kaeni kwenye mstari wenu. Dini zetu zote zinasema mamlaka yote yamewekwa na Mungu iwe mwanamke au mwanaume. Mungu ndiye anajua kwa nini Samia yupo hapa. Majoho yenu yaoneshe sura halisi. Hakuna kitabu cha dini kilichosema kitumie dini kuvuruga nchi,” alisisitiza.
Amehitimisha kwa kuwataka viongozi wa kidini na wananchi wote kulinda umoja wa kitaifa na kuepusha misuguano inayoweza kuhatarisha amani ya Tanzania.
According to a security report prepared for the United Nations, armed groups known as “bandits” in northwest Nigeria kidnapped “at least 25 residents” in twin assaults on the villages of Unguwar Tsamiya and Dabawa in Kano state.
The magnum of 1961 Dom Perignon Vintage could fetch between 500,000 and 600,000 Danish kroner ($78,000 and $93,000) at the December 11 auction in a Copenhagen suburb, the auction house said.
Several MEPs spoke about the violent crackdown on protesters, the imprisonment of nearly all major opposition leaders and the treatment of activists from Kenya and Uganda who were beaten and tortured for observing Tundu Lissu’s trial.
The state police commissioner said the attackers were herders who had “shot sporadically” during the Monday night raid on the village of Isapa, which neighbours another village where 35 people were kidnapped just a week before.
Mwasilishaji wa ombi hilo, wakili Juan Carlos Gutierrez, anayewakilisha waathiriwa, anadai kwamba Rais Samia Suluhu Hassan, kama Amiri Jeshi Mkuu, anabeba jukumu la mwisho kwa madai hayo, akisema aliidhinisha moja kwa moja matumizi ya nguvu dhidi ya raia.
The Foundation said Tanzania deserves a path toward justice, truth and national unity, calling for an honest and inclusive national dialogue.
CNN reported that bodies of protesters killed during the post-election unrest may have been buried secretly, citing satellite images, doctors’ accounts and video evidence
Waathiriwa, wengi wao wakiwa hawana silaha, walipigwa risasi na polisi, miili yao ikitupwa kama takataka. Mwanamke mjamzito ambaye alijikuta katikati ya vurugu alifyatuliwa risasi mgongoni wakati akijaribu kukimbia. Daktari aliyewahudumia majeruhi aliripoti muundo wa kutisha wa majeraha ya risasi, hasa kichwani, tumboni, kifuani na kwenye miguu.