Tanzania Opposition Rejects Election Results, Calls for Fresh Poll
“The October 29 election is null and void and all results must be cancelled,” Heche said, adding that Tanzanians were denied a genuine chance to choose their leaders.
“The October 29 election is null and void and all results must be cancelled,” Heche said, adding that Tanzanians were denied a genuine chance to choose their leaders.
Opposition party Chadema’s deputy chairperson John Heche told reporters that Tanzania witnessed “mass killings of more than 2,000 people and over 5,000 injured in the space of just one week”.
A Rwanda-backed militia late Wednesday seized control of most of the city of Uvira, the last government stronghold in the mineral-rich eastern Democratic Republic of Congo’s South Kivu province.
Human Rights Concern-Eritrea (HRCE) welcomed the release last week of 13 people, including an ex-Olympian and former police officers, who had been imprisoned for nearly 18 years without charge, trial, or access to a lawyer.
The review comes amid growing international scrutiny following the EU Parliament’s resolution calling for accountability and the release of political prisoners.
“I am hereby announcing my full and unconditional PARDON of beloved Texas Congressman Henry Cuellar … I don’t know you, but you can sleep well tonight — Your nightmare is finally over!” Trump said on his Truth Social platform on Wednesday.
Ayachi Hammami, a rights activist and staunch critic of President Kais Saied, was among some 40 Tunisian opposition figures sentenced last week up to 45 years for “conspiracy against state security” and “belonging to a terrorist group”
Uamuzi huo umetolewa leo Jumatano Disemba 3, 2025 na Hakimu Mkazi Mkuu, Aaron Lyamuya, baada wakili wa Serikali, Titus Aron kuileleza Mahakama hiyo kuwa Mkurugenzi wa Mashtaka nchini Tanzania( DPP) hana nia ya kuendelea na mashtaka shidi ya washtakiwa hao wawili.
Rais Samia Suluhu Hassan amesema sifa ya Tanzania kama kisiwa cha amani imeanza kuporomoka kutokana na matukio ya vurugu, uchochezi na matumizi ya dini katika siasa, akisisitiza kuwa vitendo hivyo vinadhoofisha misingi iliyoiweka nchi hiyo kwenye heshima ya kimataifa kwa miongo mingi.
Rais wa Tanzania Samia Suluhu Hassan amesema tofauti za kisiasa au mapenzi binafsi kwa kiongozi haziwezi kuwa sababu ya kuvuruga amani ya nchi, akisisitiza kuwa Tanzania imejengwa katika misingi ya demokrasia na utulivu tangu kuanzishwa kwake.
Akihutubia wazee wa Dar es Salaam leo, Rais Samia amesema kuwa Serikali ya Awamu ya Sita imeendelea kuboresha huduma za jamii na uchumi, na kwamba wanaoeneza chuki dhidi yake hawapaswi kutumia misingi ya dini au ukabila kuibua mgawanyiko.
“Hata kama aliyepo juu ya Serikali humtaki, kuna muda. Hii ni nchi ya kidemokrasia; huyu mtu ataongoza hadi kipindi hiki. Kama amefanya kosa, lisemeni kosa la kuongeza huduma bora za afya? Au kujenga mashule mazuri? Au kukuza uchumi hadi kusifiwa duniani? Kosa letu ni nini?” alihoji.
Ameongeza kuwa kutopenda kiongozi hakupaswi kuwa kichocheo cha vurugu: “Kama mtu hampendi anayeongoza, tustahimili tu. Ataongoza, ataondoka. Wote walioongoza tangu awamu ya kwanza, je, wote walipendwa? Kulikuwa na vurugu? Kama haumpendi Samia kwa sababu ya dini yake au alikotoka, hakuna sababu ya kuvuruga nchi.”
Rais Samia pia aliwaonya wananchi dhidi ya kile alichokiita “sumu za kisiasa” zinazoenezwa kwa jina la dini, akisema mbinu hizo hujenga chuki na kuharibu umoja wa taifa.
“Niwaombe sana: zile sumu zinazotiwa huko, mnapotiwa sumu tumieni akili zenu. Hakuna eneo baya la kumpata mtu kama dini; ukimlisha ubaya unajenga chuki moyoni. Wanasiasa wanamuharibu mtu kichwani,” alisema.
Katika wito mahsusi kwa viongozi wa dini, Rais Samia aliwahimiza kudumisha misingi ya maadili na kushikilia nafasi yao kama walinzi wa amani ambapo moja kwa moja alilitaja Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania(TEC), ambao mara kadhaa wamekuwa wakitoa waraka mzito dhidi ya mamlaka.Rais Samia alisema baraza hilo limekuwa likitoa matamko mara kwa mara, ikiwemo manane yaliyotolewa katika kipindi kifupi. Hata hivyo, amesema hata ndani ya TEC kuna viongozi wanaopinga matamko hayo wakiyaita batili, jambo analosema linaonesha kuwa msimamo huo si wa taasisi nzima.
“Viongozi wa dini kaeni kwenye mstari wenu. Dini zetu zote zinasema mamlaka yote yamewekwa na Mungu iwe mwanamke au mwanaume. Mungu ndiye anajua kwa nini Samia yupo hapa. Majoho yenu yaoneshe sura halisi. Hakuna kitabu cha dini kilichosema kitumie dini kuvuruga nchi,” alisisitiza.
Amehitimisha kwa kuwataka viongozi wa kidini na wananchi wote kulinda umoja wa kitaifa na kuepusha misuguano inayoweza kuhatarisha amani ya Tanzania.