Samia akiri ghasia za uchaguzi zimeiathiri Tanzania Kimataifa, ahofia kutopata mikopo
Rais Samia amesema Tanzania kwa kiasi kikubwa bado inategemea mikopo kutoka taasisi za Kimataifa ili kuendeleza miradi yake ya maendeleo. Hata hivyo, kutokana na matukio yaliyotokea wakati na baada ya uchaguzi, huenda taasisi hizo zikapungukiwa na imani ya kuifadhili Tanzania. Ameeleza kuwa sasa ni muhimu kutafuta mbinu mbadala za kupata fedha, ikiwemo kutumia rasilimali za taifa zilizo ndani ya nchi.