Kampeni za urais Tanzania kuanza rasmi huku mgombea wa ACT Wazalendo akizuiwa kugombea
Kwa mujibu wa INEC, jumla ya vyama 18 vilivyosajiliwa vitashiriki uchaguzi huu, na wagombea 17 wa urais watashiriki kinyang’anyiro
Kwa mujibu wa INEC, jumla ya vyama 18 vilivyosajiliwa vitashiriki uchaguzi huu, na wagombea 17 wa urais watashiriki kinyang’anyiro
Ahadi hiyo imetolewa jana katika mazungumzo yake na Rais wa Chama cha Wanasheria Tanganyika (TLS), Boniface Mwabukusi, yaliyofanyika Ikulu ya Chamwino jijini Dodoma.
Katika taarifa yake kwa umma, chama hicho kimeeleza kuwa hatua ya Msajili haina mashiko ya kisheria kwa kuwa mchakato wa uchaguzi tayari umeshaanza, huku Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC) ikiwagawia wagombea fomu za kugombea urais. Kwa mujibu wa ACT Wazalendo, Msajili hana mamlaka ya kuingilia hatua hiyo, zaidi ya kushughulikia malalamiko kwa njia ya pingamizi.
Tume ya Afrika ya Haki za Binadamu na Watu (ACHPR) imeitolea wito Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuhakikisha inalinda, inaheshimu na inatekeleza kwa dhati viwango vya haki za binadamu kuelekea uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika mwezi Oktoba 2025.
Kipindi cha uongozi wake kama Spika kiligubikwa na malalamiko kutoka kwa baadhi ya wanasiasa wa upinzani waliomtuhumu kwa upendeleo, kufungia wabunge waliokuwa wakikosoa serikali, pamoja na kuziba mijadala mizito ndani ya Bunge.
Ingawa majina ya mwisho ya wagombea yataamuliwa na ngazi za juu za chama hicho, matokeo ya sasa yameweka uelekeo wa wazi kuwa sehemu kubwa ya wanachama wameonyesha hamu ya kuona sura mpya zikipewa nafasi ya uongozi.
Katika kesi hiyo iliyopo mbele ya Hakimu Mfawidhi wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Franco Kiswaga , Lissu amedai kwamba kuendelea kwa hatua za kuahirisha kusomwa kwa shauri hilo ni dhihirisho la namna vyombo vya sheria vinavyoweza kutumiwa kisiasa, jambo ambalo ni hatari kwa mustakabali wa demokrasia nchini.
Jaji Mwanga amekuwa akisimamia kesi hiyo tangu ilipotajwa kwa mara ya kwanza mnamo Aprili 17, 2025. Hata hivyo, Juni 23 mwaka huu, walalamikaji walimuandikia barua ya kumtaka ajitoe katika kesi hiyo, wakidai upendeleo na mgongano wa kimaslahi.
Gambia imeripoti mlipuko wa ugonjwa wa mpox siku ya Jumanne baada ya kugunduliwa kwa kisa kimoja kupitia mfumo wa kawaida wa ufuatiliaji wa magonjwa, huku nchi kadhaa jirani zikiripoti ongezeko la maambukizi hivi karibuni.
Wakati wengi walitarajia angerejea katika ulingo wa kisiasa kwa mtindo mpya, Mbowe amebaki kivuli cha kile kilichowahi kuwa sauti kali ya upinzani Tanzania.