Askofu Gwajima ajiripua..aibua orodha ya Waliotekwa, ataka mabadiliko ya mfumo wa Usalama
Mbunge huyo ambaye pia ni kiongozi wa dini, ameibua msururu wa matukio ya utekaji wa raia, akisisitiza kuwa vitendo hivyo haviendani na utamaduni wa Tanzania. Ameeleza kuwa amekuwa akipokea taarifa za matukio ya utekaji, ambapo amesema kuna orodha ya takribani watu 83 waliowahi kutekwa katika miaka ya hivi karibuni.