Chadema yabaini kikosi kazi kinachohusika na utekaji nchini Tanzania, Polisi Kanda Maalum Dar yaongoza genge hilo.
Chama Kikuu cha Upinzani nchini Tanzania chama cha Chadema, kimesema utekaji unaoendelea nchini humo kwa zaidi ya asilimia 60 unafanywa na Jeshi la Polisi kupitia kikosi kazi maalum kilichoandaliwa kwa kazi hiyo.