Mwanasiasa mkongwe wa Uganda Miria Matembe aripotiwa kutekwa Kampala
Mwanasiasa mkongwe wa Uganda na mtetezi wa haki za wanawake, Miria Matembe, mwenye umri wa miaka 72, ameripotiwa kutekwa na watu wanaodhaniwa kuwa maofisa wa usalama baada ya kujificha kwa siku mbili kufuatia msako uliofanywa nyumbani kwake eneo la Luzira, jijini Kampala.