Wanajeshi wa Uganda na wa DR Congo washirikiana kukabiliana na waasi wa ADF

Rais wa Congo Felix Tshisekedi ameidhinisha wanajeshi wa Uganda kuingia DR Congo kusaidia kupambana na kundi la waasi la ADF

0
Wanajeshi wa Uganda People’s Defence Forces UPDF

Jeshi la Uganda la UPDF limeanzisha mashambulizi ya pamoja ya anga na mizinga dhidi ya kundi la waasi la Allied Democratic Forces mashariki mwa Congo.

Mashambulizi hayo yalifanywa na wanajeshi wa Congo dhidi ya kambi za ADF, msemaji wa Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Uganda Brigedia Jenerali Flavia Byekwaso alisema kupitia Twitter. Hakuna maelezo zaidi yaliyotolewa.

Hatua hiyo ya pamoja ya kijeshi inakuja muda mfupi baada ya Rais wa Congo Felix Tshisekedi kuidhinisha wanajeshi wa Uganda kuingia nchini Congo kusaidia kupambana na kundi la waasi linalodaiwa kuhusika na mashambulizi mashariki mwa Congo ambayo yamesababisha vifo vya zaidi ya watu 1,000 katika kipindi cha miaka kadhaa iliyopita. Mashambulizi yamekuwa ya mara kwa mara katika miezi ya hivi karibuni.

Takriban raia wanne waliuawa chini ya wiki mbili zilizopita katika mji mkuu wa Uganda Kampala wakati washambuliaji wa kujitoa mhanga walipojilipua kwa bomu  katika maeneo mawili.

Kundi la Islamic State lilidai kuhusika na milipuko hiyo, likisema ilitekelezwa na Waganda.

Mamlaka ya Uganda ililaumu kundi la waasi la Allied Democratic Forces kwa mashambulizi hayo. ADF ni kundi la itikadi kali ambalo limekuwa likishirikiana na kundi la IS tangu mwaka 2019.

Katika kikao cha bunge siku ya Jumanne, Serikali imetakiwa kueleza kuhusu taarifa ya kutumwa kwa Jeshi la Wananchi wa Uganda (UPDF) katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo.

Akizungumzia suala hilo kama suala la umuhimu wa kitaifa wakati wa kikao cha Jumanne, Mbunge wa Manispaa ya Mityana ambaye pia ni Kamishna wa Bunge, Francis Zaake, alisema serikali ilipaswa kupata kibali kutoka kwa Bunge kabla ya kutumwa kwa wanajeshi hao.

Hata hivyo, katika kujibu maswali ya wabunge kiongozi mkuu wa serikali Thomas Tayebwa alifafanua kuwa serikali bado inashirikisha DR Congo kuhusu hilo.

“Tunashirikisha mamlaka za Congo kuhusu uwezekano wa jeshi la UPDF kutumwa nchini Congo,” Tayebwa alisema.

Hivi majuzi, iliibuka kuwa serikali ya Uganda iliidhinishwa na DR Congo kupeleka vikosi vyake kupigana na Allied Democratic Forces.

ADF ilianzishwa mwanzoni mwa miaka ya 1990 nchini Uganda. Jeshi la Uganda baadaye liliwalazimisha waasi hao kuenda mashariki mwa Congo, ambako makundi mengi ya waasi yana uwezo wa kufanya kazi kwa sababu serikali kuu ina udhibiti mdogo huko.

In this article

East Africa Premier News Source with Top Stories, Special Features and more.
Uncensored & Undaunted