Wanamgambo wa waua 18 mashariki mwa DR Congo

mashambulizi ya CODECO yamesababisha mamia ya vifo na kusababisha zaidi ya watu milioni 1.5 kukimbia makazi yao

0

Watu 18 waliuawa siku ya Jumanne katika shambulio lililofanywa kaskazini mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo na CODECO, wanamgambo wa kikabila, afisa wa eneo hilo na mwanaharakati wa kiraia alisema.

Innocent Matukadala, mkuu wa eneo la utawala la Banyali Kilo katika jimbo la Ituri, aliiambia AFP kuwa watu 18 wameuawa na wanamgambo wa “CODECO.”

“Watu wana hasira. Mvutano ni mkubwa lakini tunajaribu kutuliza mambo,”alisema.

“Washambuliaji walitumia panga, mishale, bunduki. Watoto saba na wanawake sita walikuwa miongoni mwa wahasiriwa,” alisema Jean-Robert Basiloko, ambaye anawakilisha mashirika ya kiraia huko Banyali Kilo.

Duru zinasema kuwa, wanajeshi wa kulinda amani wa Umoja wa Mataifa na makundi ya misaada ya kibinadamu yaliondoka katika eneo hilo, lililoko katika eneo la Djugu, wiki kadhaa zilizopita.

CODECO — Ushirika wa Maendeleo ya Congo – ni kundi la kisiasa na kidini ambalo linadai kuwakilisha maslahi ya kabila la Lendu.

Jamii za Lendu na Hema zimekuwa katika mzozo wa muda mrefu ambao ulisababisha maelfu ya vifo kati ya 1999 na 2003 kabla ya mzozo huo kuingiliwa kati na kikosi cha kulinda amani cha Ulaya.

Ghasia zilianza tena mwaka wa 2017, zikilaumiwa kwa kuibuka kwa CODECO.

Tangu wakati huo, mashambulizi ya CODECO yamesababisha mamia ya vifo na kusababisha zaidi ya watu milioni 1.5 kukimbia makazi yao, wakati nusu ya wakazi wa eneo hilo wakikabiliwa na uhaba wa chakula, kulingana na Danish Refugee Council.

Watu 62, hasa kutoka Hema, waliuawa mapema Februari wakati watu waliokuwa na mapanga waliposhambulia kambi ya watu waliokimbia makazi yao.

Mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo ni nyumbani kwa makundi mengi yenye silaha, mengi yakiwa makundi yaliyoanzishwa katika miaka ya 1990.

Katika tukio tofauti usiku wa Jumapili, watu saba waliuawa katika jimbo jirani la Kivu Kaskazini na Allied Democratic Forces (ADF), chanzo cha ndani kilisema.

Shambulio hilo lililenga kijiji cha Ndiva, alisema Odette Zawadi, mwakilishi wa NGOs huko Watalinga katika eneo la Beni.

“Magaidi wanne wa ADF”waliuawa, msemaji wa jeshi la Congo katika eneo hilo, Kapteni Anthony Mualushayi, alisema.

Kundi la Islamic State linaelezea ADF,kuwa  kundi kinalojihusisha na umwagaji damu zaidi katika eneo hilo, kama mshirika wake wa ndani.

Eneo la Ndiva liko kilomita tisa (maili tano) kutoka makao makuu ya ujumbe wa kijeshi wa Uganda nchini DRC.

Wanajeshi wa Uganda waliingia nchini humo Novemba 30 katika operesheni ya pamojana vikosi vya Congo dhidi ya ADF.

Chini ya vikosi hivyo, nyadhifa za juu za kiraia katika majimbo zimechukuliwa na jeshi au ofisi za polisi, kwa nia iliyotangazwa kuharakisha vitendo dhidi ya vikundi vyenye silahaLicha ya hatua hiyo, mashambulizi yanaendelea.

In this article

East Africa Premier News Source with Top Stories, Special Features and more.
Uncensored & Undaunted