Kenya: Raila Odinga azindua manifesto yake anapowania kiti cha rais

Mgombea urais wa muungano wa Azimio Raila Odinga Jumatatu alizundua manifesto yake yenye ahadi 10, akiahidi kuinua uchumi ndani ya siku 100 za uongpzi wake kama Rais wa...

0
Mgombea urais wa muungano wa Azimio la Umoja, Raila Odinga akizungumza jukwaani wakati wa uzinduzi wa manifesto ya chama jijini Nairobi kabla ya uchaguzi wa Agosti 9 mwaka huu, Juni 6, 2022. (Photo by Simon MAINA / AFP)

Mgombea urais wa muungano wa Azimio Raila Odinga Jumatatu alizundua manifesto yake yenye ahadi 10, akiahidi kuinua uchumi ndani ya siku 100 za uongpzi wake kama Rais wa Kenya.

Akizungumza wakati wa hafla ya jioni  katika uwanja wa Nyayo, pia aliahidi kupunguza gharama ya maisha haraka iwezekanavyo na kuleta ukuaji wa uchumi

Katika kutoa manifesto yake, Waziri Mkuu huyo wa zamani pia aliahidi kuhamisha kutoa KSh6,000 kwa mwezi kwa familia zisizojiweza katika siku zake 100 za kwanza.

Aliahidi pia elimu ya bure kuanzia shule za chekechea hadi chuo kikuu,na pia kwa mafunzo ya kiufundi.

“Manifesto hii inajumuisha matumaini na matarajio ya watu wetu, na inaelezea jinsi wangependa shughuli za serikali kutekelezwa kwa niaba yao,” Raila alisema.

Kinara huyo wa chama cha ODM anawania kiti cha rais kwa mara ya tano baada ya kuwania miaka ya 1997, 2007, 2013 na 2017 bila mafanikio.

Katika uzinduzi huo Raila aliangazia hatua za kipaumbele ambazo alisema zitabadilisha maisha ya Wakenya.

Raila aliahidi serikali yake itapambana na ufisadi, kuongeza huduma za afya kwa wote na kupanua nafasi ya kujieleza kwenye vyombo vya habari.

Akiwa rais, Raila alisema, ataongeza ufadhili kwa kaunti 47 za kaunti, kuhakikisha usalama wa chakula, kupatikana kwa maji kwa kila nyumba na kuongeza nafasi za kazi.

Alisema njia mojawapo itakuwa ni utambuzi wa vyeti vya awali vya ujifunzaji kwa mafundi waliohitimu.

Hiyo itawapa fursa ya kupata kandarasi za serikali na kazi zaidi.

Raila alisema ataangazia mipango ambayo itawaepusha sana Wakenya kutoka kwa gharama ya juu ya maisha ambayo imefanya maisha ya mamilioni ya raia kuwa magumu.

Huduma ya afya kwa wote itatekelezwa katika muda wa miezi mitatu baada ya kuchaguliwa kwake, alisema.

Alisema watumishi wote wa umma waliostaafu wataendelea kupokea bima ya matibabu kwa gharama ya serikali.

Kuhusu vita dhidi ya ufisadi, Raila alisema wanachama wote wa Azimio – walioteuliwa na kuchaguliwa – watatia saini hati maalum ya kupambana na ufisadi kwamba hawatajihusisha na ufisadi wa aina yoyote

Odinga alisema ataliagiza Bunge kuanzisha mbinu za kuwezesha uchunguzi wa haraka, mashtaka na kesi za ufisadi.

Raila aliahidi kuimarisha taasisi zinazopambana na ufisadi, kuboresha uratibu wao na kutumia mbinu na teknolojia za kibunifu kukabiliana na ufisadi.

Anapanga pia kuanzisha sera za kudhibiti adhabu na hukumu kwa wakosaji kwa misingi ya uwiano.

Odinga alisema atahakikisha kila mtoto anapata elimu kupitia mpango wake wa elimu ya bure wa ‘Waste No Child.’

Mpango huo pia utashughulikia wanafunzi wa vyuo vikuu na taasisi za mafunzo ya ufundi stadi.

Hivi sasa, serikali inatekeleza elimu ya msingi bila malipo kwa wote na elimu ya sekondari ya malipo kidogo.

Wanafunzi wa vyuo vikuu wanaweza kupata mikopo ili kuwezesha elimu yao.

Raila pia alisisitiza mpango wake wa Baba Care utaleta mageuzi katika sekta ya afya kwa kuwapa Wakenya wote nafasi ya kupata huduma za afya za msingi.

Raila, ambaye mpinzani wake wa karibu ni Naibu Rais William Ruto, alifichua manifesto yake kwa Kenya siku moja baada ya kupitishwa na shirika la uchaguzi kuwania urais.

.

In this article

East Africa Premier News Source with Top Stories, Special Features and more.
Uncensored & Undaunted