IGP Wambura, DCI Kingai, CDF Mkunda Kuja Kutoa Utetezi Dhidi ya Lissu
Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam imekubali ombi la Mwenyekiti wa CHADEMA, Tundu Lissu, la kuwaita Mkuu wa Jeshi la Polisi Tanzania IGP Camilius Wambura, Mkurugenzi wa Makosa ya Jinai DCI Ramadhani Kingai na Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama CDF. Generali Jacob John Mkunda, kuwa mashahidi wa upande wa utetezi katika kesi ya uhaini inayomkabili.